Dr. Lorah Madete akimpongeza mmoja wa Mwenyekiti- Mwenza wa Kikundi Kazi Mwakilishi wa Hungary Balozi Csaba Korosi mwishoni wa mkutano wa 11 wa kikundi kazi hicho. Pembeni anaonekana Mwakilishi wa Kenya, Balozi Macharia Kamau ambaye pia ni Mwenye Kiti- Mwenza wa kikundi hicho
Balozi Tuvako Manongi, Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, akijiandaa kuwasilisha mchango na maoni ya Tanzania wakati wa Mkutano wa kumi na Moja wa Kikundi Kazi cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Kikundi Kazi hicho ambacho Tanzania ni mjumbe kilikutana wa wiki moja ambapo kilipitia na kuboresha rasimu ya malengo mapya ya maendeleo baada ya 2015. Walio kaa nyuma wa Balozi ni Dr. Lorah Madete, Afisa Mkuu kutoka Ofisi ya Rais-Tume ya Mipango na Bw. Noel Kangada Afisa wa Uwakilishi wa Kudumu
Na Mwandishi Maalum
Kikundi kazi cha Baraza Kuu la Umoja wa
Mataifa kilichopewa jukumu la
kupendekeza Malengo Mapya ya Maendeleo Endelevu
baada ya 2015 ( SDGs) kimemaliza mkutano
wake wa kumi na moja kwa kupitisha
maazimio mbalimbali.
Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania ni kati ya nchi 30 zinazounda kikundi kazi hicho na imeendelea
kushiriki kikamilifu katika kuhakikisha kwamba, matakwa ya nchi maskini na
zinazoendelea yanazingatiwa ipasavyo katika maandalizi ya malengo hayo mapya ambayo yatachukua
nafasi ya Malengo ya Maendeleo ya Millenia ( MDGs).
Wajumbe wa Kikundi kazi hicho walikutana kwa wiki moja hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, na kazi kubwa iliyofanyika katika wiki hiyo
moja, ilikuwa ni kupitia na kuboresha
rasimu ya malengo mapya ya
maendeleo iliyokuwa imeandaliwa na Wawakilishi wa Kudumu wa Kenya na Hungary
ambao ni Wenyeviti -Wenza wa Kikundi
Kazi hicho.
Rasimu hiyo ilijumuisha
maeneo muhimu yaliyomo kwenye Malengo ya
Millenia na ambayo yanahitaji msisitizo
na msukumo zaidi katika mpango mpya wa maendeleo baada ya 2015. Maeneo hayo ni
pamoja na kuondoa umaskni, kuhakikisha upatikanaji wa chakula, afya, elimu na uwezeshaji wa wanawake.
Aidha maeneo mapya
yanayojumuishwa ni pamoja na upatikanaji
wa maji safi na salama, nishati,
miundombinu, utunzaji wa mazingira
yakiwamo ya baharini, kuhakikisha
usawa miongoni na baina ya nchi, na ujenzi wa jamii zenye amani,
zinazotingatia utawala bora na utawala wa sheria
Akichangia majadiliano
ya uboreshaji wa rasimi hiyo, Balozi Tuvako Manongi, Mwakilishi wa Kudumu
wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,
na ambaye aliongoza ujumbe wa Tanzania
katika mkutano huo, alisisitiza umuhimu
wa uwezeshaji makini wa nchi
maskini na zinazoendelea.
Balozi Manongi alieleza
kuwa nchi maskini na zinazoendelea
zinapashwa kuwezeshwa ili kupitia
uwezeshwaji huo basi ziweze kuwa katika
nafasi nzuri ya kutekeleza malengo mapya ya maendeleo kama
ili vyokubalika katika Mkutano wa
Kimataifa wa Maendeleo Endelevu uliofanyika Rio de Janeiro, Brazil mwaka 2012.
Aliyataja maeneo ambayo
nchi maskini na zinazoendelea zinahitaji uwezeshwaji makini kuwa ni pamoja na , masuala ya biashara ambapo nchi zilizoendelea zinatakiwa kupunguza vikwazo vinavyozinyima nchi
zinazoendelea kufaidi fursa za biashara
ya kimataifa.
Vile vile Tanzania imezitaka nchi zilizoendelea kuzisaidia nchi maskini kujenga uwezo wa kuendesha sekta muhimu kama vile kilimo, uchukuzi, viwanda, elimu na afya, sekta ambazo Tanzania inaamini ni muhimu kwa maendeleo.
Katika mkutano huo
wa kumi na moja na ambao pia Asasi zisizo
za Kiserikali zilipata pia fursa ya kuwasilisha mapendekezo yao.
Tanzania pia imezitaka nchi
zilizoendelea na zinazoibukia kiuchumi kuzipatia nchi maskini teknolojia
salama na uelewa utakazoziwezesha kuongeza kasi ya maendeleo nchi zao.
Balozi Manongi
akiwasilisha maoni ya Tanzania, pia alisisitiza
suala la upatikanaji wa
fedha za
ndani mathlani kupitia ukusanyaji wa mapato. Pamoja na misaada na uwekezaji kutoka nje katika kufanikisha utekelezaji wa
malengo hayo.
Kikundi kazi kinatarajiwa kuhitimisha shughuli zake
Julai 2014 kwa kuwasilisha taarifa yake kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,
ambaye naye ataiwasilisha taarifa hiyo
kwenye Kikao cha 69 cha Baraza kuu la Umoja wa Mataifa mwezi
Septemba 2014.
Taarifa hiyo pamoja
na taarifa za michakato mingine kuhusu
agenda ya maendeleo baada ya 2015,
itakuwa ndio msingi wa majadiliano ya nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa yatakayohitimishwa mwezi Septembea 2015
katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali ambapo wanatatarajiwa kupitsha agenda hiyo na
malengo ya maendeleo endelevu ambayo
ndiyo mrithi wa Malengo ya sasa ya
Millenia.

No comments:
Post a Comment