ANGALIA LIVE NEWS

Wednesday, July 16, 2014

Pistorius ajikuta pabaya klabuni

Mwanariadha wa Afrika Kusini anayekabiliwa na kesi ya mauaji, Oscar Pistorius, amedaiwa kuhusika katika malumbano ndani ya klabu moja nyakati za usiku mwishoni mwa wiki.

Mwanariadha huyo alikuwa katika klabu moja alipojikuta katika hali ya majibizano makali na mfanyabiashara mmoja aliyekuwa amemuuliza kuhusu kesi anayokabiliwa nayo.

Mfanyabiashara huyo Jared Mortimer anayedaiwa kumshambulia Oscar kwa maneno akimuuliza kuhusu kesi yake, anasema kuwa Pistorius alikuwa mlevi chakari wakati wa majibizano hayo.

Sarakasi hiyo ilitokea katika klabu ya kifahari mjini Sandton kufuatia madai kuwa Pistorius aliwatusi marafiki wa Jared Mortimer pamoja na kuitusi familia ya Rais wa Afrika Kusini Jaocb Zuma.

BBC

No comments: