Advertisements

Thursday, August 21, 2014

KAMPUNI YA TANZANIA DISTILLERIES LTD (TDL) YAZINDUA KINYWAJI KIPYA CHA KIMATAIFA, FYFE’S SCOTCH WHISKY KATIKA SOKO LA TANZANIA

 Mkurugenzi mtendaji wa TDL David Mgwasa akielezea na kutoa ufafanuzi wa Kinywaji kipya aina ya Fyfe's.Kampuni ya Tanzania distilleries ltd (tdl) Juzi Tarehe 20 mwezi wa 8 2014 imefanya uzinduzi wa kinywaji chake kipaya aina ya  Fyfe's katika hoteli ya Serena, Kinywaji hicho ambacho uhalisia wake na uzindikaji ni wa nchini scotland.Mkurugenzi wa TDL David Mgwasa amewaomba waTanzania kukipokea kinywaji hicho kwenye soko la vimiminika kwani kina ubora wa hali ya juu na kimetengenezwa kwa asilimia kubwa kwa kutumia vitu asilia,

 Langas Group wakiingia ukumbuni kwa kutoa burudani ikiwa ni kumkaribisha Bwana Langa Khanyile ambaye ni mtaalamu wa masuala ya upishi wa bia na uchanganyaji.

 Langa Khanyile mtaalamu wa upikaji na uchanganyaji wa kinywaji cha Fyfe’s akicheza kwa furaha na mshehereshaji wa shughuli hiyo Jimy Kabwe Ndani ya Serena Hotel wakati wa uzinduzi

 Langa Khanyile mtaalamu wa upikaji na uchanganyaji wa kinywaji cha Fyfe’s akitoa maelezo ya kina ni kwa namna gani kinywaji hicho kinaandaliwa kutoka hatua ya kwanza mpka Mwisho.
Moshi mkubwa ukitoka ndani ya kifaa cha mfano wa glass ya asili kuashiria uzinduzi rasmi wa kinywaji cha Fyfe’s ndani ya Serena hotel
 Wageni waalikwa na wadau mbalimbali wakiangalia namna pekee ya uzinduzi wa kinywaji cha Fyfe’s

                      Na Hatimaye Kinywaji kikawa tayari kimezinduliwa Rasmi
 Wahudumu wa Serena Hotel wakigawa glass zenye kinywaji cha Fyfe’s ili kuweza kujionjea Ladha yake
Cheeers hapo ni wageni waalikwa na wadau mbali mbali wakifurahia ladha ya kinywaji cha Fyfe’s mara tu baada ya kuonja,
Wageni waalikwa na wadau mbalimbali wakifuatilia kwa umakini Uzinduzi wa kinywaji cha Fyfe’s
 Langa Khanyile mtaalamu wa upikaji na uchanganyaji wa kinywaji cha Fyfe’s akifurahi pamoja na wadau na wageni waalikwa
 Uonjaji na unywaji wa kinywaji cha Fyfe’s   kwa wadau na wageni mbalimbali
 Meneja Masoko wa TDL akitoa ufafanuzi wa bei za kinywaji aina ya Fyfe’s  pamoja na kuchezesha draw ya bahati na sibu kwa wageni na  wadau waliofika kwenye uzinduzi huo
 Mshindi wa Kwanza kwenye uzinduzi wa bia ya Fyfe’s  Bwana Bernard Suma maarufu magodoro akifurahia ushindi wa kwanza ambapo atakwea pipa moja kwa moja mpka Scotland kwa ajili ya kujione namna kinywajui hicho kinavyotengenezwa.
 Langas Group wakitooa burudani ya asili kutoka nchini scotland kwa wageni na wadau mbalimbali
Wageni wakiendelea kubadilishana mawazo pamoja na kunywa kinywaji cha Fyfe’s

1 comment:

Anonymous said...

uhuru wa bendera huu kwani hakuna vinywaji vya makabila menginewe hapo nchini kama vile waganga kwa nini wasiboreshe mbega yao na wengi wengi tu.
inatuhusu nini au inagusa maisha yetu yapi kwa kinywaji hii,imekuwa Tanzania dampo la kina biashara za nje na utamaduni wa nje.
ndo maana mwalimu nyerere alikuwa hataki mambo haya alikuwa ameona mbali sana mzee yule mungu amrehemu,amen.
sasa tume kuwa kama watumwa wao na tuna uhuru wa bendera tuu.

tunapangiwa sherehe chungu nzima mwisho itafika tutakuwa hatuna hata usemi katika nchi yetu na ardhi yote itamilikiwa na wao.mungu tusaidiye.