Advertisements

Friday, August 22, 2014

SERIKALI YATOA UFAFANUZI MALIPO YA MISHAHARA YA WATUMISHI YA MWEZI JULAI


Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati alipokuwa akifafanua juu ya malipo ya mishahara ya watumishi yaliyofanyika mwezi Julai mwaka huu leo jijini Dar es salaam ambapo ameonya mamlaka husika ziwe na taarifa sahihi za idadi ya watumishi ili kuondoa makosa ya kulipa mishahara hewa, endapo kutatokea makosa ya ulipaji wa mishahara hewa watachukuliwa hatua za kisheria na kufikishwa mahakamani.
(Picha zote na Eleuteri Mangi – MAELEZO)

No comments: