Advertisements

Wednesday, September 24, 2014

LORI LAPINDUKA NA KUUA WANNE MBEYA

WATU WANNE WAMEFARIKI DUNIA NA WENGINE KUJERUHIWA BAADA YA GARI LENYE NAMBA ZA USAJILI T.200 AKQ AINA YA ISUZU LORI IKIENDESHWA NA DEREVA ASIYEFAHAMIKA KUACHA NJIA NA KISHA KUIGONGA PIKIPIKI YENYE NAMBA ZA USAJILI T.614 BUK AINA YA T-BETTER ILIYOKUWA PEMBENI YA BARABARA NA KISHA KUPINDUKA.
AJALI HIYO ILITOKEA MNAMO TAREHE 22.09.2014 MAJIRA YA SAA 17:00 JIONI HUKO MLIMA NYIMBILI, KATA NA TARAFA YA KAMSAMBA, BARABARA YA KAMSAMBA/MLOWO, WILAYA YA MOMBA, MKOA WA MBEYA.
WALIOFARIKI KATIKA AJALI HIYO NI 1. SELA MKISI (30) MKAZI WA NTUNGWA 2. ENEA MGALA (42) MKAZI WA NKANGA 3. LUSIANO MTENDA (50) MKAZI WA MKOMBA NA 4. ELITA MASHAKA (02) MKAZI WA NTUNGWA. 
AIDHA WATU KADHAA WALIJERUHIWA NA WAMELAZWA KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA MBOZI VWAWA KWA MATIBABU. MIILI YA MAREHEMU IMEHIFADHIWA KATIKA HOPSPITALI YA KAMSAMBA WILAYA YA MOMBA. CHANZO CHA AJALI KINACHUNGUZWA. DEREVA ALIKIMBIA MARA BAADA YA TUKIO NA JUHUDI ZA KUMTAFUTA ZINAENDELEA.

No comments: