Advertisements

Friday, December 19, 2014

TANZANIA YASISITIZA AZIMIO KUHUSU WATU WENYE ULEMAVU WA NGOZI LIWE NA TIJA

.Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi akilizungumza Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa hapo siku ya Alhamis kabla Baraza hilo halijapigia kura Azimio linalotaka kuwapo kwa siku ya Kimataifa ya kuwatambua watu wenye ulemavu wa ngozi. Kulia kwa Balozi ni Bi. Ellen Maduhu Afisa wa Uwakilishi anayeshughulika Kamati ya Tatu inayohusika na masuala ya Haki za Binadamu, Utamaduni na Masuala ya Jamii na alishiriki kikamilifu katika majadiliano ya kwanza kuhusu Azimio hilo ambapo alihakikisha Azimio limetambua juhudi zinazofanywa na Serikali katika kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ngozi pamoja na kuzikabili changamoto wanazokumbana nazo.
Sehemu ya Wajumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa wakiwa katika mkutano ambao ulipitisha maazimio mbalimbali yaliyowasilishwa mbele ya Baraza hiyo na Kamati ya Tatu. Baadhi ya Maazimio yaliyopitishwa katika mkutano huo uliofanyika siku ya Alhamis lilikuwapo linalopendekeza kuwapo wa siku ya Kimataifa ya watu wenye ulemavu wa ngozi ( Albino).

Na Mwandishi Maalum, New York

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  imesisitiza kwamba haitoshi kuwa na siku ya kimataifa ya kuwatambua watu wenye ulemavu wa ngozi ( Albino)   pasipo  kuwa na mikakati madhubuti  inayolenga katika kuwawezesha.
 Hayo yameelezwa na  Mwakilishi wa  Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi alipokuwa akizungumza muda mfupi kabla ya  Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa  halijapigia kura   Azimio linalotaka kuwepo kwa Siku ya Kimataifa ya  Kuwatambua watu wenye Ulemavu wa ngozi.
Leo ( Alhamsi) Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa  lilipokea mapendekezo  ya maazimio mbali mbali yaliyowasilishwa mbele ya Baraza  hilo  yakitokea  Kamati ya Tatu ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Kamati inayohusika na masuala ya Haki za Binadamu,  Utamaduni na Maendeleo ya Jamii.
Miongoni mwa Maazimio hayo lipo lililohusiana na Haki za Binadamu  ambapo ndani ya  maazimio ya eneo hilo kuna   azimio   linalopendekea  kuwa  wa siku ya kimataifa ya watu wenye ulemavu wa ngozi.
Balozi Manongi  amelieleza Baraza hilo kuwa, kimsingi Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, haipingi kuwapo kwa  siku ya kimataita ya kuwatambua watu wenye ulemavu wa ngozi .  Lakini  inapata shida pale azimio hilo linaposhindwa  kuainisha  mchango  na mikakati ya kimataifa ya  kuwezesha  jamii hiyo  kukabiliana na changamoto mbalimbali.

 Akiongea kwa msisitizo, Balozi Tuvako  Manongi ameeleza kuwa  Tanzania  ni nchi ambayo inaidadi kubwa ya watu wenye ulemavu wa ngozia na pamoja na  changamoto na matatizo wanayokumbana nayo.
Amezitaja  baadi ya changamoto hizo  na ambazo pia zimeainishwa  katika Tume ya Haki za Binadamu kuwa ni  pamoja na kutopata   huduma kamilifu  za kiafya,  elimu, kunyanyapaliwa na  madhira mengine.
 “Kuna changamoto mbalimbali  zinazowakabili,    Changamoto ambazo zinatakiwa kufanyiwa kazi na kutafutiwa ufumbuzi.  Kama nchi yenye idadi kubwa ya watu wenye  ulemavu wa ngozi, Ujumbe wangu ulijjitahidi  katika kuhakikisha  kuwa pendekezo la Azimio hili ambalo leo limeletwa mbele ya Baraza hili linakuwa lenye tija na manufaa zaidi kwa walengwa kuliko lilivyo hivi sasa” amesema Balozi Manongi
Amesema   kuwa  pamoja na  kwamba pendekezo hilo la kuwa na siku ya kimataifa ya watu wenye ulemavu wa ngozi ni hatua muafaka, lakini halitoi mwelekeo wa  namna ya kushughulikia  matatizo yao  pamoja na  uwezeshwaji wao.
Ni kwa sababu  hiyo  na kutokana na mapungufu hayo ambayo yalikuwa hayatoi nafasi wa Jumuiya ya Kimataifa kushirikiana na Juhudi za  Tanzania katika kuzikabili changamoto zinazowakabili watu wenye ulamemavu wa ngozi.Ndiyo maana Tanzania kwa nia njema kabisa  iliomba azimio hilo  lipigiwe  kura si kwa maana ya kulipinga azimio lakini kupinga azimio hilo kutokuwa na maslahi  mapana kwa watu wenye ulemavu wa ngozi.
Mwakilishi huyo wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, amekwenda mbali zaidi  kwa kusema kuwa  Tanzania  na kama ilivyokuwa kwa wanachama wengine,  imekuwa ikiaamini kuwa Chombo hicho kwa maana ya  Baraza Kuu la Umoja wa  Mataifa na Umoja wa Mataifa kwa ujumla wake vinapashwa kupitisha maamuzi na maazimio yenye tija zaidi.
Azimio hilo limepitishwa kwa kupigiwa kura ambapo licha  ya mapungufu yake,  inatambua kuwa  June 16  ya kila mwaka itakuwa ni siku ya Kimataifa ya kuwatambua watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino)


No comments: