Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Jan Eliasson akizungumza wakati wa uzinduzi wa mfumo mpya wa thathmini na utambuzi wa viashiria vinavyoweza kama visipodhibitiwa mapema kuleta uhalifu, uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita. uzinduzi huo umefanyika siku ya Alhamisi hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa
Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Balozi Ramadhan Mwinyi akizungumza wakati wa hafla hiyo ambayo iliandaliwa kwa pamoja na Wakilishi za Kudumu za Tanzania na Italia katika Umoja wa Mataifa pamoja na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuzuia mauaji ya Kimbari na Wajibu wa Kulinda Raia
Sehemu ya Washiriki wa uzinduzi huo ambapo mkazo mkubwa ulikuwa ni ushiriki wa wadau wengine kama vile vyombo vya habari na asasi zisizo za kiserikali na wajibu wao katika utambuzi wa viashiria vya uvunjifu wa amani na hatua mbalimbali ambazo vyombo hiyo vinaweza kusaidia kuzuia uvunjifu huo
Na Mwandishi Maalum, New York
Imeelezwa kuwa waandishi wa habari pamoja na vyombo
wanavyofanyia kazi wana nafasi kubwa ya ama kuchochea uibukaji wa
machafuko katika nchi zao au kuyazuia
kwa kutumia kalamu zao.
Hayo yameelezwa siku
ya Alhamis hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa wakati wa hafla ya uzinduzi wa
mfumo mpya wa uchambuzi unaolenga kutathmini viashiria hatarishi vya uhalifu, mauaji ya kimbari ,uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu
wa kivita
Hafla ya uzinduzi wa
mfumo huo ambao umeandaliwa kwa ushirikiano baina ya Ofisi ya Umoja wa Mataifa kuhusu Mauaji ya
kimbari na Ofisi ya Umoja wa Mataifa
kuhusu wajibu wa kuwalinda raia (R2P) iliandaliwa kwa ushirikiano wa Wakilishi za Kudumu za
Tanzania na Italia katika Umoja
wa Mataifa na Ofisi ya Umoja wa Mataifa kuhusu uzuiaji wa mauaji ya Kimbari na
ulinzi wa Raia. Uzinduzi uliohudhuriwa
na Naibu
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Jan
Eliasson.
Mfumo huo( framework of
Analysis for Atrocity Crimes, a tool for prevention) pamoja na mambo
mengine licha ya kutoa ufafanuzi, tafsri
na maelezo ya kina kuhusu viashiria na
mazingira ambayo yanaweza kupelekea
au kusababisha mauaji ya halaiki au kimbari, uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa makosa ya kivita unapanua wigo wa kuvishirikisha vyombo vya
habari na asasi za kiraia kama wadau
muhimu wa si tu kufanya tathmini ya awari ya viashiria hivyo lakini ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua za mapema za kuuzia kuibuka kwa
matatizo hayo katika jamii.
Vyombo vya habari na Asasi za kiraia vinaelezwa kama wadau
muhimu licha ya ukweli kwamba wajibu wa kwanza wa kuzuia
machafuko ya aina yoyote ile pamoja na
kutoa ulinzi wa raia ni wa
serikali kuu.
Na kwa sababu hiyo
imeshauriwa kuwa waandishi wa habari wanapashwa kwanza
kutambua vyema viashiria
hatarishi dhidi ya Amani na usalama na kuwa nyenzo muhimu ya kuzuia kuibuka
kwa uhalifu huo badala ya kuwa sehemu ya uhalifu huo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mfumo huo, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Jan Eliasson amesema ,
mwaka 2014 umeshuhudia umwagaji
mkubwa wa damu kuliko miaka mingine yoyote.
Amesema hali hiyo
inatoka na ama kwa Jumuiya ya Kimataifa
kutotambua mapema na katika hatua za awali
za dalili ya kutokea uhalifu na
uhalifu dhidi ya binadamu au ni kwa jumuiya
ya kimataifa kutofautiana kimtazamo na kimaslahi kuhusu njia muafaka za
kuzuia uhalifu huo.
Akasema uzinduzi wa
mfumo huo unatoa fursa kwa serikali na
wadau wengine ya kutambua mapema
viashiria vya uwepo wa mazingira hatarishi yanayoweza kusababisha mauaji ya
kimbari, uhalifu dhidi ya binafamu na
uhalifu wa kivita. Lakini kubwa na la msingi anasema ni kuzuia uhalifu huo kabla haujatokea.
Amesisisitiza kuwa uhalifu
dhidi ya binadamu hauibuki mara moja,
bali ni jambo linalokuwa limepangwa na
kuandaliwa kwa muda mrefu
ukiwashirikisha wadau mbalimbali.
Amesema hali
ilivyo hivi sasa ni kwamba jumuiya ya
kimataifa imejikuta ikijikita zaidi katik a kushughulikia matatizo ambayo tayari
yameshajitokeza badala ya kuyazuia
katika hatua za awali hali
inayosabibisha kutumia gharama kubwa zaidi.
Kwa upande wake Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika
Umoja wa Mataifa, Balozi Ramadhan Mwinyi, pamoja na kuelezea umuhimu na manufaa ya mfumo huo wa tathmini ya
viashiria vya uwepo wa
mazingira hatarishi. Amesema Tanzania inaunga mkono ushirikishwaji wa
wadau mbalimbali kama sehemu
muhimu katika eneo zima la Amani, usalama na ulinzi wa raia.
Hata hivyo ametahadharisha kuwa pamoja na kutambua mchango wa
wadau wengine, ni vema basi pawepo na utaratibu
wa uwajibikaji wa wadau hao ikiwa ni pamoja
usimamizi lengo likiwa ni
uwajibikani kama baadhi ya wadau
hao wanakuwa chanzo au chachu cha machafuko hayo.
Aidha Balozi
Mwinyi amesema Tanzania ni rafiki wa
mchakato huo wa wajibu wa kuwalida raia (R2P). Lakini ni ukweli usionpingika kuwa dhana hiyo ya
wajibu wa kuwalinda raia bado
imegubikwa na utatamwingi na kwamba kwa nchi nyingi hususani za afrika
bado dhana hiyo haijakubalika au haijapokelewa vema.
Amesema sababu ya kutopokelewa vema kwa dhana hiyo na
waafrika kunatokana na ukweli kuwa dhana hiyo inalenga zaidi katika kuingilia
masualaya ndani ya nchi husika na pia ni
dhana inayolenga katika kuleta mabadiliko ya kiuongozi katika nchi husika ( regime change).
Na kwa sababu hiyo, Mwakilishi huyo wa Tanzania katika Umoja
wa Mataifa amesisitiza haja na umuhimu wa kuwapo na usimamizi na utambuzi
maalumu kuhusu dhana hiyo ya wajibu wa kulinda raia bila ya kuingilia
uhuru wa nchi husika.
Katika uzinduzi huo, baadhi ya wachangiaji wa mfumo huo
wa thathmini pamoja na dhana ya R2P akiwamo Katibu Mkuu
Msaidizi Mwandamizi anayehusika na masuala ya
uzuiaji wa mauaji ya kimbari, Bw. Adama Dieng wameielezea Tanzania kama nchi ambayo ni
kielelezo halisi cha Amani, usalama na utulivu ikilinganishwa na mataifa mengine Barani Afrika.
Akizungumzia wajibu wa vyombo vya habari katika kuzuia
machafuko ambayo yanaweza kupelekea
kutoka kwa matukio ya uhalifu na makosa ya jinai dhidi ya binadamu. Bi, Agnes
kut Callamard kutoka Chuo Kikuu cha Columbia. Amesisitiza haja na umuhimu kwa waandishi wa habari kuzingatia maadili ya kazi zao huku akitilia mkazo utendaji kazi huru wa vyombo hivyo ikiwa ni pamoja na haki ya kupata habari na kusambaza habari.
Amesisitiza kuwa
uzoefu umeonyesa kuwa sehemu
nyingi ambapo kumetokea machafuko,
vyombo vya habari vimebainika kuchangia
kwa asilimia kubwa uwepo wa hali hiyo.
Naye B.i Peggy Hicks kutoka Human Rights Watch akizungumzia kuhusu nafasi ya asasi
zisizo za kiserikali pamoja na mambo mengine amesema kuwa Tanzania ina mfumo mzuri unaoziwezesha asasi zisizo za kiserikali
kutekeleza majukumu yao pasipo kuingiliwa sana na serikali kuu. Na kusisitiza
asasi hizo za tanzania hazihitaji
kujifunza kutoka nje juu ya utekelezaji wa majukumu yao.
Aidha katika uzinduzi
huo Tanzania imeelezwa pia kuwa Taifa ambalo
kumekuwapo na ustawi,
maridhiano na kuvumiliana kwa hali ya juu baina ya
madhehebu mbalimba ya dini.
No comments:
Post a Comment