Advertisements

Sunday, January 25, 2015

AZAM FC, SIMBA SC NGUVU SAWA TAIFA

TIMU ya Simba SC na Azam FC zimeshindwa kutambiana leo katika mechi ya Ligi Kuu Bara baada ya kutoka sare ya bao 1-1.

Katika mechi hiyo iliyopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar, bao la Simba limefungwa na Emmanuel Okwi dakika ya 19 wakati la kusawazisha la Azam likifungwa na Kipre Tchetche dakika ya 57.

Mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi alitolewa uwanjani kwenye machela baada ya kuzimia uwanjani alivyogongana na Aggrey Morris wa Azam kukimbizwa hospitali.

No comments: