Advertisements

Sunday, January 25, 2015

VIONGOZI WA DINI, MAIMAMU KUIENDELEZA JAMII

Sheikh Amir Kundecha (kulia) akizungumza jambo, kushoto ni Sheikh, Rajabu Katimba.
…akionyesha baadhi ya nyaraka na gazeti lenye habari za Waislam.
Baadhi ya Maimamu wakiwa kwenye kongamano hilo.
Sheikh Rajabu Katimba akizungumza na wanahabari (hawapo pichani)

BARAZA Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania, leo katika ukumbi wa Lamada, jijini Dar es Salaam, limefanya kongamano lililowahusisha viongozi wa dini na Maimamu katika kuiendeleza jamii.

Akizungumza kwenye kongamano hilo, Katibu wa Baraza hilo Sheikh Rashidi Katimba alisema; “Hatutakuwa tayari kuupigia kura ya ndiyo mchakato wa Katiba mpya inayopendekezwa kama serikali na viongozi hawataki kuweka baadhi ya mahitaji ya Waislam tuliyopendekeza ikiwemo Mahakama ya Kadhi na mengineyo.

(Picha na Gabriel Ng’osha/GPL)

1 comment:

Anonymous said...

mambo ndo haya mpango mzima hatutaweza kuipigia kura ya NDIO,wasitufanye wajinga waislamu tumeshachoka kunyanyaswa na kudharauliwa kila siku miaka yote. imepoa sana kitu hichi baridi hakina noma.waislamu oyeeeeeeeeeee.

Allah awe na nyinyi daima amin thuma amin.