Advertisements

Tuesday, March 3, 2015

DKT. TITUS KAMANI ATEMBELEA MAONESHO YA KIMATAIFA YA KILIMO NCHINI UFARANSA

Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi,Mhe. Dkt. Titus Kamani akitembelea mabanda ya maonesho ya kimataifa ya kilimo yanayofanyika katika Jiji la Paris nchini Ufaransa,na kujionea aina ya mifugo inayoshindanishwa. Hapa anaangalia ng'ombe wa nyama aina ya Charolaise.
Mhe. Dkt. Kamani akiangalia kondoo wa sufi waliopo kwenye mabanda ya maonesho.
Umati wa watu kutoka mataifa mbalimbali duniani waliohudhuria maonesho hayo. Takriban watu milioni moja wametembelea maonesho hayo kwa mwaka huu 2015 ambayo hufanyika kwa muda wa siku tisa.
Mhe. Dkt. Kamani pamoja na ujumbe wa watanzania wakisikiliza kwa makini maelezo ya maendeleo ya sekta ya mifugo nchini Ufaransa na mfumo wa uendeshaji wa maonesho ya kimataifa ya kilimo kabla ya kupata fursa ya kutembelea mabanda mbalimbali.

No comments: