Advertisements

Wednesday, March 4, 2015

Rais Kikwete amtembelea Rubani wa ndegevita Hospitali ya Jeshi Lugalo

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma wakimjulia hali Meja Peter Lyamuya aliyelazwa katika hospitali kuu ya jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam akiuguza jeraha la mguu alilopata baada ya ndege ya kivita aliyokuwa akiiendesha kuanguka na kulipuka wiki iliyopita.Askari huyo wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) alinusurika kifo baada ya kufanikiwa kujiokoa katika ajali hiyo iiyosababishwa na ndege mnyama kuingia kwenye injini na kusababisha hitilafu iliyopelekea kushika moto, kuanguka na kulipuka.Ndege hiyo ilikuwa katika mazoezi ya kawaida kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza.(picha na Freddy Maro)

3 comments:

Anonymous said...

Really ? jama kavunjika mguu raisi anaenda kumtembelea ?

Anonymous said...

Huyo ndio rais wetu mdau hapo juu,hata ukifanya birthday ukimualika atakuja tu

Anonymous said...

Hata kupaka rangi ukuta nayo ni issue? Hii Bongo ya Le Mutus kazi kwelix2.