Hivi karibuni kumekuwa na matukio
mbalimbali kwa upande wa chama kikuu cha upinzani CHADEMA
kinachonisukuma kusema kuwa tunachoona hivi sasa ni historia. Bila
kupoteza muda mrefu kujaribu kuzungumzia matukio naona kuwa watanzania
tungefaidika zaidi kuelewa vyema zaidi nini hasa tunachokiona.
Lazima tukubali kuwa lengo moja kuu
(kama si lengo kuu pekee) ya chama chochote cha kisiasa ni kuingia
madarakani. Vyama hivi vinaweza kutushawishi kuwa wanataka madaraka haya
kwa sababu wanataka kutusaidia na ni haki na wajibu wetu kutathmini na
kuamua ni chama kipi kitatusaidia kama jamii kufikia malengo
tutakayokubaliana nayo. Lakini kwa kifupi wanataka madaraka.
Tukishakubali hali hii, basi tunaweza kuangalia tukio lolote la kisiasa
kama ushindani wa kutwaa madaraka. Na ni muhimu tutambue hili bila
kujaribu kudai kuwa eti mwanasiasa au chama fulani kinatupenda na
kutujali zaidi na kadhalika. Hilo ni suala la mtazamo na kwa sasa
tuliweke pembeni.
Ninachotaka tujaribu kuangalia ni kuwa
ushindani huu wa kutwaa madaraka pia yapo ndani ya chama chochote cha
kisiasa. Na ni kitu kizuri sana. Naamini ndani ya CCM, CHADEMA, CUF,
NCCR tutaendelea kuona malumbano kwa sababu ya uchaguzi mkuu 2015. Ni
uchaguzi wa kihistoria kwa sababu rais aliyopo madarakani hatagombea
tena (hakuna incumbent) hivyo hata mgombea wa CCM atakuwa ‘mgeni’ kwa
wapiga kura. Hivyo vyama vya upinzani vina nafasi kubwa sana wakicheza
karata zao vizuri. Lakini pia ndani ya CCM, hakuna mteule mpaka sasa –
kwa hiyo yoyote anaweza kuibuka kuwa mgombea. Tukishaweza kuangalia hali
ya kisiasa kwa jicho hili tutaona kuwa ndani ya vyama kuna makambi
ambayo yanaona kuwa wao wakiendesha chama sasa wanaweza kukihakikishia
ushindi chama chao. Hivyo uongozi wa chama nao unawaniwa. Na ninarudia
hakuna ubaya wowote tena ni kitu kizuri. Kwani asiyekubali kushindana si
mshindani – na ukweli ni kuwa mgombea ambaye atateuliwa tu na chama
chake bila kupitia ushindani mkubwa ndani ya chama chake, mara nyingi
hawi mgombea mwenye ushwawishi mkubwa. Kusoma zaidi bonyeza HAPA
No comments:
Post a Comment