Advertisements

Thursday, July 30, 2015

RAIA WAKIGENI 2040 WAKAMATWA WAKIWA NA VITAMBULISHO VYA KUPIGIA KURA

Kaimu kamishna wa uhamiaji Abasi Irovya akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo, kuhusiana na wahamiaji haramu wanayo jiandikisha katika  Daftari la wapiga kura katika mikoa mbalimbali hapa nchini.
Kutoka kushoto ni Naibu Kamishna wa uhamiaji wilaya ya Iala, Safina Muhindi,katikati ni Afisa  uhamiaji wilaya ya Temeke, Jaffari Kisesa na Afisa Mdhibiti wa Paspoti, Cripin Ngonyani wakimsikiliza Kaimu kamishina wa uhamiaji Abasi Irovya wakati akizungumza na waandishi wa habari leo katika ukumbi wa mikutano ofisini kwao jijini Da es Salaam leo.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Kaimu kamishna wa uhamiaji Abasi Irovya jijin Dar es Salaam leo. Picha na Avila Kakingo.


Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
Raia wa kigeni wajaribu kujipatia vitambulisho vya kupigia kura wafikia 2040 kwa mikoa ya  mikoa ya Kagera watu 708, Mara 619, Tanga 348,Kigoma 254, Rukwa 13, Kilimanjaro 12, Ruvuma 9, Geita 6, Shinyanga 7, Mtwara 3, Pwani 2, Mbeya 1, Morogoro 1 na Dar es Salaam 65. 
Hayo yamesemwa na Kaimu kamishna wa uhamiaji Abasi Irovya wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano ofisini kwao  jijini Dar es Salaam leo.

 Aidha Irovya amesema amewakumbusha wananchi kupiga kura ni haki ya kila mwananchi wa Tanzania ana sio raia wa kigeni kujiandikisha ili apige kura kwana raia wa kigeni hana uwezo wa kupiga kura katika nchi asiko zaliwa.

Pia Irovya amesema kuwa wananchi walio chukua paspoti za kusafiria zinapoisha muda wake ni lazima wabadilishe na kupewa nyingine wakati wowote wanapohitaji.
  
 Irovya ameongezea kuwa wananchi wanaotafuta paspoti za kusafiria tofauti na ofisi za uhamiaji wajue huko wanapotea paspoti zote zinapatikana katika ofisi za uhamiaji tuu na sio popote pale.

3 comments:

Anonymous said...

Hii ninkitu isiyokubalika kabisa ni vyema tume na wahusika uhamiaji wawe makini na hata wakati wa kupoga kura. Je ni hatua gani imechukuliwa kwa hawa waliokamatwa. Isiishie hewani tuuh

Anonymous said...

Tatizo ni kwamba tunayo mipaka ambayo siyo rahisi kuilinda i.e. porous borders. Cross-border movements of people from neighboring countries, needs to be thoroughly examined and controlled. Kuna hatari kubwa, kwani tunasikia Wa-nigeria wengi wamepata njia za kupenyeza mipakani na kuingia Bongo kama udagaa!

Anonymous said...

watu wa UKAWA hao eti nia ya kuingia IKULU,

HATA MFANYEJE HAMPATI HATA ROBO YA KURA,

SUBIRINI MAGOLI YA MIKONO MUYAONE YA MARADONA CHA MTOTO