Advertisements

Wednesday, August 26, 2015

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO AFUNGUA KONGAMANO LA WADAU WA FAMILIA

 Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii , Jinsia na Watoto Mhe.Dkt  Pindi Chana (Mb) akiangalia baadhi ya machapisho yanayohusiana mbinu za malezi na makuzi ya watoto kabla ya kufungua semina ya siku mbili ya matokeo ya utafiti wa malezi na makuzi ya familia nchini iliyofanyika Hotel Protea Courtyard, jijini Dar es salaam.
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii  Jinsia na Watoto  (Mhe. Dkt  Pindi Chana (Mb) akifungua rasmi   Kongamano la siku mbili la wadau wa familia wanaokutana kupokea matokeo ya utafiti wa malezi na makuzi ya watoto katika familia lililofanyika hotel Protea jijini Dar es salaam, tarehe 26/8/2015.
Kauli mbiu ni ‘FAMILI BORA TAIFA IMARA AULI MBIU’.
Kulia; Naibu Waziri Mhe.Dkt  Pindi Chana (Mb)akisikiliza maelezo ya utangulizi ya Kongamano la Utafiti wa Malezi na Makuzi  ya Watoto katika Familia (kushoto) ni Kaimu Katibu Mkuu  wa wizara hiyo Bibi Nuru Millao aliyeongozana na Mhe. Naibu Waziri katika ufunguzi wa kongamano la kitaifa la familia katika hotel ya Protea, jijini Dar es salaam tarehe 26/8/2015
 Baadhi ya washiriki wa Kongamano la Utafiti wa Malezi na Makuzi ya Watoto katika Familia wakifuatilia kwa makini hotuba ya ufunguzi iliyotolewa na Mhe. Dkt. Pindi Chana (MB hayupo pichani) katika Hotel ya Protea Courty yard jijini Dar es salaam tarehe 26/08/2015.

No comments: