ANGALIA LIVE NEWS

Tuesday, September 8, 2015

MSAFARA WA JAMES MBATIA WAISIMAMISHA VUNJO

Msafara wa Pikipiki ukimsindikiza mgombea Ubunge katika jimbo la Vunjo kupitia chama cha NCCR-Mageuzi na UKAWA ,James Mbatia wakati wa kwenda kufanya uzinduzi wa Kampeni katika jimbo jilo.
Msululu wa magari ukimsindikiza mgombea huyo.
Maeneo mbalimbali aliyopita mgombea huyo alipokelewa na makundi mbalimbali ya watu waliokuwa wamesimama kando ya barabara wengi wao wakiwa ni kina mama.


Katika maeneo mengine wananchi walisimamisha msafara wake na kusalimia kwa muda kabla ya kuendelea na safari.
Shughuli zilisimama kwa muda katika maeneo mbalimbali angalau kutoa nafasi japo kupunga mkono kwa mgombea huyo.
Msafara ukielekea uwanja wa Michezo wa Chuo cha Ualimu cha Marangu kwa ajili ya uzinduzi wa mkutano wa Kampeni.
Makondakta na madereva wa daladala katika eneo la Marangu mtoni wakisalimiana na mgombea ubunge katika jimbo la Vunjo ,James Mbatia.
Hii ndivyo ilivyokuwakatika eneo la Marangu Mtoni.
Raia wa kigeni wakichukua taswira za mgombea Ubunge katika jimbo la Vunjo,Jmaes Mbatia.
Mgombea Ubunge katika jimbo la Vunjo James mbatia kaiwa ameongozana na mkewe ,Catherine Mbatia na motto wao Chelsea wakiingia katika uwanja wa michezo wa chuo cha Ualimu Mrangu kwa ajili ya mkutano wa ufunguzi rasmi wa kampeni. Na Dixon Busagaga

1 comment:

Anonymous said...

MHESHIMIWA JAMES MBATIA TAYARI AMESHAPITA JIMBO LA VUNJO YAANI MBUNGE WA KUCHAGULIWA JIMBO LA VUNJO KUANZIA TAREHE 26 OCTOBA 2015 KAAPISHWA BUNGENI DODOMA NA SPIKA MPYA MHESHIMIWA JAMES LEMBELI AISEE KAITWA IKULU NA MHESHIMIWA EDWARD NGOYAI LOWASSA RAIS MPYA WA AWAMU YA TANO [2015-2020] MMM UTAMU JUU YA UTAMU KATEULIWA NA MHE. RAIS KUWA WAZIRI MPYA WA ELIMU NA WALIMU HONGERA SANA SANA MHESHIMIWA MBATIA SASA CHAPA KAZI IRUDISHE HADHI YA ELIMU TANZANIA,UBARIKIWE EEEMIN.