Advertisements

Friday, October 2, 2015

ESMA: NAMSHANGAA SANA DIAMOND!


Dada wa ‘kichaa’ wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Esma .

Brighton Masalu
DADA wa ‘kichaa’ wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Esma amemshangaa kaka yake, (Diamond) kwa kuendeleza chuki dhidi ya baba yake mzazi, mzee Abdul Jumaa.Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu hivi karibuni, Esma alisema siku zote si vyema kukaa na kinyongo au chuki dhidi ya wazazi na hata kama ikitokea ni vyema kuyamaliza kwa mtoto kujishusha.
“Hata mimi nilishawahi kukosana na baba yangu, lakini nilishasamehe na kusahau kabisa, hata hapa nyumbani, ni mara nyingi tu huwa tunatofautiana na mama lakini hata kama yeye kakosea, huwa najishusha si kama ilivyo kwa Nasibu (Diamond) kuwa na chuki kali kiasi hicho dhidi ya baba yake,” alisema Esma.
source:GPL

2 comments:

Anonymous said...

Labda tukushangae wewe unayejitoa public kuingilia mambo yasiyokuhusu!

Anonymous said...

Mambo yenu ya nyumbani sio ya kuyaweka kwenye public.Starabika dada..