Meneja kutoka Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Kanda ya Mashariki Bw. Daniel Ndiyo akiwaeleza waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kuhusu mpango wa kudhibiti majanga yatokanayo na kemikali ambapo Serikali inaendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu madhara ya kemikali hatari kwa binadamu na mazingira. Kulia ni Afisa Habari wa ofisi hiyo Bw. Sylvester Omary
(Na Jovina Bujulu- MAELEZO)
Kukosekana
kwa uelewa juu ya hatari na madhara yanayoweza kusababishwa na kemikali
kumetajwa kuwa ni chanzo kikubwa cha ajali mbali mbali hapa nchini.
Hayo yamesemwa jijini Dar es salaam na Meneja wa Kanda ya Mashariki wa Wakala wa
Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Ndugu Daniel Ndiyo alipokuwa
akizungumzia utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi
na uthibiti wa kemikali.
“Chanzo
kikubwa cha ajali na matukio mengi ya kemikali yanayotokea yanatokana na
kukosekana kwa uelewa juu ya hatari na madhara yanayoweza kusababishwa na
kemikali hizo”
“Ajali
hizo zinaweza kuzuilika endapo wananchi watapatiwa elimu na uelewa wa matumizi
au usimamizi sahihi na salama wa kemikali hizo” alisema ndugu Ndiyo.
Akizungumzia
ajali hizo, kwa kipindi cha mwaka 2014, ndugu Ndiyo alitoa mfano wa matukio na
ajali zipatazo 11 zilizotolewa taarifa
ambazo zilisababisha vifo vya zaidi ya watu 14
pamoja na uharibifu mkubwa wa mali ikiwemo kuungua moto kwa magari na
tani zaidi ya 250 za kemikali.
Akizungumzia hatua za utekelezaji, usimamizi na udhibiti
wa wa kemikali ndugu Ndiyo alisema kuwa sheria na kanuni ya kemikali ya mwaka
2015, inaagiza kuwa kila anayehusika na kemikali kwa kuingiza kutoka nje,
kusafirisha, kuuza, kusambaza, kutumia au kwa namna yoyote ile ni lazima awe
amesajiliwa na Mkemia Mkuu wa Serikali nchini.
Aidha
Ndugu Ndiyo alisema kuwa baada ya kupitishwa kwa sheria na kanuni za kemikali
kumekuwa na mafanikio mbali mbali ikiwa ni pamoja na udhibiti wa kemikali zinazoingizwa
nchini tangu usafirishaji, utumiaji na hata uteketezaji wake.
“Hatua
hii imesaidia kutambua mapema kemikali zinazoingia nchini, mahali zinapokwenda
na matumizi yake, hatua ambayo imesaidia kuzuia kemikali hatarishi ambazo
zinaweza kuleta madhara kwa watu na mazingira kuingia na kutumika nchini”
aliongeza ndugu Ndiyo.
Sheria
ya Usimamizi na Udhibiti wa kemikali za
Viwandani na Majumbani Sura 182 ilitungwa ili kuhakikisha kuwa kemikali
zinatumika katika hali iliyo salama bila kuleta athari kwa watu na mazingira.
No comments:
Post a Comment