Advertisements

Wednesday, October 7, 2015

Mkutano wa vyama vinavyounda UKAWA Wawi, Chakechake Pemba

MGOMBEA urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Wananchi CUF Mhe: Maalim Seif Sharif Hamad akivishwa koja, kabla ya kuzungumza na mamia ya wanachama wa vyama vinavyounda UKAWA, uliofanyika Ditia Jimbo la Wawi wilaya ya Chake chake Pemba.
MJUMBE wa baraza kuu taifa la chama cha CHADEMA Janeth Madadi Fussi, akitoa salamu zake kwa mamia ya wanachama wa vyama vinavyounda UKAWA, kwenye mkutano uliofanyika Ditia, Jimbo la Wawi wilaya ya Chake chake Pemba, na kuhutubiwa na mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF maalim Seif Sharif Hamad.
WANACHAMA wa CUF na wengine wanaounda UKAWA, wakifuatilia hutuba ya mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF maalim Seif Sharif Hamad, akizungumza kwenye mkutano wa kuwanadi wagombea wa majimbo ya Chake chake na Wawi pamoja na wadi zake.
KADA wa chama cha wananchi CUF bwana Sanya akizungumza kwenye mkutano wa kuwanadi wagombea wa Majimbo ya Chake chake na Wawi na wadi zake, uliofanyika uwanja wa Ditia Jimbo la Wawi na kuhutubiwa na mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya chama hicho, maalim Seif Sharif Hamad.
MGOMBEA urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF Maalim Seif Sharif Hamad, akimnadi mgombea Udiwani wa wadi ya Tibirinzi Mohamed Hafidh Ngwidi, kabla ya kuzungumza na wanachama wa chama hicho, kwenye mkutano uliofanyika Ditia Jimbo la Wawi.
MGOMBEA urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF maalims Seif Sharif Hamad, akimnadi mgombea Ubunge Jimbo la Chake chake Yussuf Kaiza Makame, kabla ya kuzungumza na wanachama wa chama hicho, kwenye mkutano uliofanyika Ditia Jimbo la Wawi.
MGOMBEA urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha wananchi CUF Mhe: maalim Seif Sharif Hamad akizungumza na wanachamawa chama hicho, kwenye mkutano wa kuwanadi wagombea wa nafasi mbali mbali wa majimbo ya Wawi na Chake chake, mkutano huo ulifanyika Ditia Jimbo la Wawi, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

No comments: