Advertisements

Wednesday, October 7, 2015

SHIGONGO ATOA SEMINA YA UJASIRIAMALI KWA WANACHAMA WA TCRA SACCOS

SHIGONGO TCRA SACCOS (8)
Eric Shigongo akifundisha somo la Sheria 10 zilizothibitishwa za jinsi ya kutoka kwenye umasikini hadi mafanikio kwa wanachama wa TCRA Saccos.
SHIGONGO TCRA SACCOS (5) SHIGONGO TCRA SACCOS (6)
SHIGONGO TCRA SACCOS (7)
Baadhi ya wafanyakazi na wanachama wa TCRA Saccos wakimsikiliza kwa makini somo la Shigongo.
shigongo
Shigongo akizidi kutoa semina kwa wanachama wa TCRA Saccos.
SHIGONGO TCRA SACCOS (1)
Mwenyekiti wa TCRA Saccos, Erasmus Mbilinyi akimkaribisha Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dkt. Ally Yahaya Simba ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi katika semina ya leo.
SHIGONGO TCRA SACCOS (2)
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dkt. Ally Yahaya Simba akitoa nasaha zake kwa wanachama wa TCRA Saccos.
SHIGONGO TCRA SACCOS (3)
Wanachama wa TCRA Saccos wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dkt. Ally Yahaya Simba.
SHIGONGO TCRA SACCOS (4)
Eric Shigongo (kushoto) akifurahia jambo wakati Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dkt. Ally Yahaya Simba akitoa nasaha zake.
y
Mmoja wa wanachama wa TCRA Saccos akitoa shukrani kwa Shigongo baada ya kulielewa vizuri somo lake.
SHIGONGO TCRA SACCOS (10)
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dkt. Ally Yahaya Simba akisoma mojawapo ya vitabu vya Shigongo.
SHIGONGO TCRA SACCOS (11)
...Hapa akiangalia CD ya Shigongo.
SHIGONGO TCRA SACCOS (12) SHIGONGO TCRA SACCOS (13)
SHIGONGO TCRA SACCOS (15)
Shigongo akiweka saini yake katika vitabu vilivyonunuliwa na wanachama wa TCRA Saccos.
SHIGONGO TCRA SACCOS (14)
Wanachama wa TCRA Saccos wakinunua CD na vitabu vya Shigongo baada ya semina.
SHIGONGO TCRA SACCOS (16)
Shigongo akibadilishana mawazo na wanachama wa TCRA Saccos.
MWANDISHI na mhamasishaji mahiri Afrika ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Global Publishers Ltd, Eric Shigongo James, leo ametoa semina ya ujasiriamali kwa wanachama wa TCRA Saccos.
Semina hiyo imefanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo Makao Makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) jijini Dar es Salaam.
Katika semina hiyo, Shigongo amefundisha somo la Sheria 10 zilizothibitishwa za jinsi ya kutoka kwenye umasikini hadi mafanikio.
Akifungua semina hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dkt. Ally Yahaya Simba ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi alieleza umuhimu wa kuwa na Saccos katika kuinua maisha ya wanachama wake. Baada ya semina hiyo kumalizika, wanachama wa TCRA Saccos walipata fursa ya kununua vitabu pamoja na CD za Shigongo zilizokuwa zikiuzwa eneo hilo.
(HABARI; CLARENCE MULISA, PICHA; PATRICK BUZOHERA / GPL)

1 comment:

Anonymous said...

kuna mdau anaye jua elimu ya shigongo.si kumkashifu ila kumfagilia nilisoma mahali kulikuwa na issue za ujasiria mali basi jamaa akasema hivi watanzania mbona tuko waogo tukiambiwa tujiunga na vijana wenzetu tusitafute ajira kwa serikali au mtu binafsi tuanzishe ujasiria mali sisi wenyewe tuna sita na kukata.
na kutoa sababu chungu nzima.ooh sina mtaji oooh sijasoma sina elimu ya kutosha je kuna mtu anajua elimu ya shigongo.ndo hapo sasa na ndo nikaja na kuliza hili swali. JE KUNA ANAYE JUA ELIMU YAKE.Nasikia si msomi lakini yupo kama msomi kwa utunzi wake mahiri.