Wednesday, December 9, 2015

NAPE AWAPA MAKATIBU KATA WA JIMBO LAKE PIKIPIKI

Mbunge wa Jimbo la Mtama Ndugu Nape Nnauye akimkabidhi Katibu wa kata ya Mtua Kilimahewa funguo ya pikipiki kwa niaba ya makatibu kata 20 wa jimbo hilo ambao wote wamewezeshwa usafiri wa pikipiki ili kurahisisha ufanisi wa kazi zao.
Mbunge wa Jimbo la Mtama (CCM) Nape Nnauye akijaribu moja ya pikipiki kati ya 20 alizowapa makatibu kata ili ziweze kuwasaidia kufanya kazi kwa ufanisi kwenye shughuli zao za kujenga na kuimarisha Chama Cha Mapinduzi.
Sehemu ya pikipiki zilizotolewa na Mbunge wa Jimbo la Mtama Ndugu Nape Nnauye kwa makatibu kata 20 wa jimbo hilo.
Mbunge wa Jimbo la Mtama Ndugu Nape Nnauye akizungumza mbele ya viongozi wa CCM wilaya ya Lindi vijijini ambapo aliwaambia viongozi hao kuwa amejipanga kufanya kazi katika jimbo hilo zenye kuleta tija na kuhakikisha anatekeleza ahadi zote alizozitoa wakati wa kampeni na kuwata makatibu kata waliokabidhiwa pikipiki 20 kuzitumia katika kazi za kujenga na kuimarisha chama.

2 comments:

Anonymous said...

Katoa wapi hizi pesa
Pikipiki zimelipiwa ushuru

Gharama tujuwe

Anonymous said...

AMEWAPA?NI ZAKE AU NI ZA CCM?KAMA NI ZAKE KATOA PESA WAPI ZA KUGAWA PIKIPIKI KAMA NJUGU? HUYU BWANA ANA FAILI TAKUKURU NA VIASHIRIA RUSHWA KWAKE NDIVYO HIVI VINADHIHIRIKA.MTAMA HATUNA MBUNGE.