Advertisements

Tuesday, February 16, 2016

Masanja Azidi Kupaa Kibiashara Azindua Masanja Wali Nyama Tabata


MCHEKESHAJI wa Komedi kutoka Orijino Komedi Emmanuel Mgaya a.k.a Masanja Mkandamizaji amezidi kujikita katika mkasuala ya biashara baada ya kufanikiwa kufungua mgahawa wa kisasa kabisa kwa ajili ya maakuli na kuwa kivutio kwa maeneo hayo.
Masanja Mkandamizaji amezindua Mgahawa wake wa Kisasa kwa kuandaa sherehe za uzinduzi kwa kuwakaribisha wadau mbalimbali Mgahawa huo unaoitwa “Masanja Wali Nyama” upo maeneo ya Tabata Magengeni Karibu na Benki ya CRDB BANK.

Shughuli hiyo iliyo anza saa mbili usiku na kumalizika saa tano usiku, ilipambwa na waimbaji mbalimbali wa muziki wa injili akiwemo Miriam Jackson, Emmanuel Mbasha, Faraja Ntaboba, Mc Makondeko, Stella Joel pamoja na Wachungaji, Mitume na Manabii.

Huku pia wakiwepo wasanii waigizaji mbalimbali ambao walifika kwa ajili ya kumsapoti msanii huyo majasirimali ambaye licha ya kumiliki mgahawa huo Masanja pia ni mkulima mzuri mwenye mashamba ya kulima Mpunga makubwa tu, hivyo amezidi kupaa zaidi Hongera sana.


No comments: