Advertisements

Saturday, February 13, 2016

MWENYEKITI WA TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA AFANYA ZIARA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Mstaafu), Damian Lubuva akieleza jambo mbele ya ujumbe wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (hauko pichani), ujumbe huo ulipoitembelea ofisi yake jana (Februari 12, 2016).


Februari 12, 2016), Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Mhe. Bahame Tom Nyanduga akiambatana na baadhi ya viongozi wa Tume hiyo ametembelea Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wake, Mhe. Jaji (Mstaafu), Damian Lubuva kuhusu uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25, 2015.

Katika ziara hiyo, Mhe. Nyanduga alipata fursa pia ya kumweleza Mhe. Lubuva kuhusu uangalizi uliofanywa na Tume katika uchaguzi huo katika Mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Lindi na Zanzibar.
Mwenyekiti wa THBUB, Mhe. Bahame Tom Nyanduga na Katibu Mtendaji wa Tume, Bibi Mary Massay wakimsikiliza kwa makini Mhe. Jaji (Mstaafu) Lubuva.
Mhe. Jaji (Mstaafu) Lubuva akimsikiliza Mhe. Nyanduga (hayupo pichani) wakati wa mazungumzo yao.
Mhe. Bahame Tom Nyanduga na Mhe. Jaji (Mstaafu), Damian Lubuva wakiwa katika picha ya pamoja na Kamishna wa Tume, Mhe. Dkt. Kelvin Mandopi na Bibi Mary Massay.
Mhe. Bahame Tom Nyanduga na Mhe. Jaji (Mstaafu), Damian Lubuva wakiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa THBUB na baadhi ya maafisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
(Picha zote na Germanus Joseph wa THBUB).

No comments: