Advertisements

Sunday, February 14, 2016

SHEREHE ZA KANISA WAADVENTISTA WASABATO MTAA WA MANZESE ZAFANA

Jeshi la vijana Watafuta Njia (PFC) wakionesha programu maalum katika sherehe ya kumuaga Mch. Amosi Lutebekela (hayupo pichani) iliyofanyika katika kanisa la waadventista wasabato Manzese jana.
Kwaya ya wasabato ya Mbiu wakikabidhi zawadi ya kwaya kwa Mch. Amosi Lutebekela na Mkewe kwenye sherehe ya kuwaaga iliyofanyika jana katika kanisa la wasabato Manzese.
Kwaya ya Wasabato Ruvu kitonga wakimtukuza Mungu kwa njia ya uimbaji wakati wa sherehe ya kumuaga Mch. Amosi Lutebekela iliyoandaliwa na kanisa la wasabato mtaa wa Manzese.

Kwaya ya Angaza wakiimba wimbo maalum wa kumuaga Mch. Amosi Lutebekela kwenye sherehe ya kumuaga iliyoandaliwa na kanisa la wasabato mtaa wa Manzese.

WASABATO WAKUMBUSHWA KUZINGATIA KIAPO CHA KUDUMU KWENYE NDOA HADI KIFO KIWATENGANISHE
Na. Sarah Reuben
Mkurugenzi wa Sauti ya Unabii, Uchapaji na Maeneo Mapya Mch. Amosi Lutebekela jana amekemea tabia mbaya ya baadhi ya waumini wa kanisa la waadventista wasabato wanaoshindwa kutimiza kiapo chao cha ndoa na kuanza kudai kuvunja ndoa kwa sababu zisizokubalika kibiblia.
Akizungumza wakati wa ibada kuu katika kanisa la waadventista wasabato Manzese, jijini Dar es Salaam, Mch. Lutebekela alisema hivi karibuni idadi ya wanandoa ambao wanaomba kuvunja ndoa inaongezeka tena kwa sababu zisizokubalika kibiblia.
“Mimi kama msajili wa ndoa nimekuwa nikishughulikia  changamoto mbalimbali za wanandoa ambao wamekuwa wakiomba kuvunja ndoa kama suluhisho la migogoro yao. Ninakemea wanandoa wote wenye malengo ya kuvunja ndoa kinyume na utaratibu wa biblia. Tabia hiyo ikome mara moja kwa jina la Yesu, alisisitiza.
Katika hotuba yake vilevile Mch. Lutebekela aliwataka vijana ambao hawajaingia katika ndoa kuzingatia sifa za kiroho zaidi badala ya kutegemea mivuto ya kimwili yaani sura nzuri na muonekano wa nje. “Ninapenda kuwaasa vijana wa kiume na wakike epukeni sana kutafuta wenzi wa maisha kwa kuangalia mivuto ya nje yaani sura na muonekano. Sura inachakaa lakini roho na tabia njema haitachakaa hata umri wenu ukisonga, alifafanua Mch. Lutebekela.
Mch. Amosi Lutebekela aliyasema hayo katika sherehe ya kumuaga rasmi iliyoandaliwa na Kanisa la Waadventista Wasabato Mtaa wa Manzese baada ya kuteuliwa kuwa mkurugenzi wa Sauti ya Unabii, Uchapaji na Injili katika maeneo mapya hivi karibuni. Kabla ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi, Mch. Lutebekela alikuwa mchungaji anayesimamia Mtaa wa Manzese.  

No comments: