Advertisements

Tuesday, May 31, 2016

MFUKO WA PENSHENI WA PPF WAHIMIZA WAKAZI WA TANGA KUJIUNGA NA MFUMO WA WOTE SCHEME

 Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Charles John Mwijage akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kutembelea banda la Mfuko wa Pensheni wa PFF mara baada ya kufungua maonyesho ya biashara ya kimataifa ya Tanga yanayofanyika kwenye viwanja vya Mwakidila jijini

 Afisa wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Mkoa wa Tanga, Jabir Bundile akiwa kwenye banda lao lililopo kwenye maonyesho hayo

Afisa wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Mkoa wa Tanga, Jabir Bundile wa pili kulia akitoa elimu kwa mkazi wa Tanga namyanatolewa na mfuko huo.
na ya mafao WAKAZI wa Mkoa wa Tanga wametakiwa kutumia fursa ya kujiunga na Mfumo wa wote scheme unaotolewa na Mfuko wa Pensheni PPF ili kuwawezesha kukithi mahitaji kwa sababu unalengo kuu la kutambua mchango wa ushiriki kwenye sekta isiyo rasmi katika kuinua uchumi.
 Hayo yalisemwa jana na Afisa wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Mkoa wa Tanga, Jabir Bundile wakati alipozungumza na gazeti hili katika maonyesho ya nne ya biashara ya kimataifa ya Tanga yanayofanyika kwenye viwanja vya Mwakidila jijini hapa ambapo alisema mfumo huo utasaidia kufikia wananchi wengi.
 Alisema kuwa fao hilo likuwa likitoa fursa mbalimbali kwa wafanyakazi waliopo kwenye sekta iliyo rasmi na isiyorasmi ili kuwawezesha kunufaika na mfumo huo kwa ajili ya kukuza shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii kwa mustakabali wa maendeleo yao. 
“Niwaambieni kila mtu au kikundi chenye mlengo wa kiuchumi kilichopo kwenye sekta isiyorasmi kama vile wakulima, wafugaji, wavuvi, mama lishe, waendesha pikipiki, wajasiriamali wadogo wadogo kwa lengo la kuhakikisha wananufaika kupitia mfumo huo “Alisema. 
Aliongeza kuwa pia mfumo huo unawagusa wasanii, wana michezo, wachimbaji madini wadogo wadogo wanaweza kujiunga na mfumo huo kwa lengo la kupata manufaa yanayotokana na mfuko huo. 
Sambamba na hilo pia alisisitiza uwepo wa mafao yanayotolewa na mfuko huo kuwa ni ule wa Afya, Fao la Uzeeni, Mkopo wa elimu ambao unalengo la wanachama kukopa na kujiendeleza kielimu na PPF na mkopo ambao unakuwezesha kutimiza ndoto yako.
Habari kwa hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

No comments: