Advertisements

Monday, May 2, 2016

SERIKALI KUFUFUA KIWANDA CHA GENERAL TYRE

Kiwanda cha kutengeneza matairi cha General Tyre mkoani Arusha kinatarajiwa kufufuliwa hivi karibuni.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Felix Ntibenda amesema jana kuwa lengo la Serikali ni kukuza uchumi kwa vijana.
Ntibenda alisema wakati akihutubia katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha.
Alisema hadi sasa Serikali inamiliki hisa kwa asilimia 100 katika kiwanda hicho na muda wowote kitaanza uzalishaji.

No comments: