Advertisements

Tuesday, May 31, 2016

VIJANA 30 MAARUFU KAMA “TEREZA”WALIOKUWA WAKIWABAKA NA KUWAJERUHI WANAWAKE WAKAMATWA

Jeshi la Polisi mkoani Kigoma limefanikiwa kudhibiti wimbi la wanawake kubakwa na kujeruhiwa na vijana wanaojulikana kama Tereza baada ya kuendesha msako na kuwakamata vijana 30 wanaotuhumiwa kuunda genge linaloendesha vitendo hivyo mitaani nyakati za usiku.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kigoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Ferdinand Mtui amesema watu hao ambao wamekamatwa katika maeneo ya Vamia Mwanga na Katubuka watafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika na kwamba wamebaini kuwa maeneo yanakotokea matukio hayo ya ubakaji hakuna umeme, nyumba nyingi hazina milango imara na maeneo hayo yamezungukwa na vilabu vya pombe.

Kwa upande baadhi ya wakazi wa mjini Kigoma,wamesema uwepo matukio hayo ya ubakaji umesababisha hofu katika jamii ambapo wamelitaka Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi zaidi wa suala hilo na kulipatia ufumbuzi wa kudumu ili kuondoa hofu katika jamii.

No comments: