Friday, June 3, 2016

RAIS DKT. MAGUFULI ATEUA MWENYEKITI MPYA WA BODI YA TPDC

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, amemteua Prof. Sufian Hemed BUKURURA kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kuanzia tarehe 30 Mei, 2016.

Kufuatia uteuzi huo, Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Profesa Sospeter M. Muhongo (Mb.), amewateua wafuatao kuwa  Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya TPDC kuanzia tarehe 3/6/2016 hadi tarehe 2/6/2019;

1. Mhe. Jaji Josephat M. Mackanja
2. Balozi Dkt. Ben Moses
3. Prof. Abiud Kaswamila
4. Prof. Hussein Hassani Sosovele
5. Dkt. Shufaa Al-Beity
6. Bi. Mwanamani Kidaya

Imetolewa na;
KATIBU MKUU 
3 JUNI, 2016

No comments: