Advertisements

Wednesday, July 20, 2016

MAANDALIZI YA MKUTANO MKUU WA CCM YAPAMBA MOYO MKOANI DODOMA

 Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Abdulrahman Kinana akielekeza jambo kwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM - Bara, Ndg. Rajab Luhwavi (mwenye koti) pamoja na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi wa CCM,Ndg. Nape Nnauye (kushoto), wakati wa maandalizi ya Mkutano Mkuu wa CCM, unaotarajiwa kufanyika Julai 23, 2016 kwenye Ukumbi wa CCM Dodoma Convention Centre, Mjini Dodoma leo. Alie nyuma ya Katibu Mkuu, ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM - Zanzibar, Ndg. Vuai Ali Vuai
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Abdulrahman Kinana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM - Bara, Ndg. Rajab Luhwavi wakiweka sawa moja ya Vibao vitakavyotambulisha Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM kutoka Mikoa yote nchini, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa CCM, unaotarajiwa kufanyika Julai 23, 2016 kwenye Ukumbi wa CCM Dodoma Convention Centre, Mjini Dodoma leo. 
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Abdulrahman Kinana akikagua Ukumbi wa CCM Dodoma Convention Centre, kutakakofanyikia Mkutano Mkuu wa CCM, unaotarajiwa kufanyika Julai 23, 2016.
Maandalizi yakiendelea.

No comments: