Advertisements

Friday, July 1, 2016

Taarifa na Shukran Za Dhati kutoka kwa Mariam Hussein Washington DC

Kwa niaba ya Mariam Hussein tunapenda kutoa shukran za dhati kwa Ndugu, Jamaa na Marafiki

wote waliojitolea kwa hali na mali, wakati wa mapambano ya Saratani ya Tumbo.

Amefarajika sana kwa michango ya pesa, waliokwenda kumuona, waliompigia simu kumjulia

hali, na kwa waliomuombea Dua kwa Mwenyezi Mungu amfanyie wepesi wakati anapambana

na Saratani ya Tumbo.

Mariam Hussein amefanyiwa upasuaji June 7, 2016 katika hospitali ya George Washington

Memorial, Washington DC kuondoa uvimbe wa saratani kwenye tumbo na sasa hivi yuko

nyumbani anaendelea vizuri na recovery. Tunamshukuru Mungu kila kitu kimekwenda sawa.

Bado yuko kwenye uangalizi wa madaktari wake na ataendelea kutumia dawa za kusaidia kuto

kurejea kwa saratani mpaka watakapoamua kuwa hazihitajiki tena.

Tunaombwa tuendelee kumuombea dada yetu kwani maombi yetu bado yanahitajika.

Tunapenda kuchukua fursa hii kuwajulisha pesa tulizopokea kutoka kwenu kumsaidia wakati wa

mapambano haya :-

Go Fund Me $8,700

Harambee $4,300

Waliotuma direct $1,500

Jumla $14,500

Mwenyezi Mungu atuzidishie imani, upendo, maelewano na ushirikiano.

Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu. 

Asanteni sana.

Kwa Taarifa Zaidi

Asha Hariz 703 624 2409

Edima Elinewinga 202-459- 1217

No comments: