Advertisements

Friday, August 12, 2016

NAIBU WAZIRI MASAUNI AZINDUA MASHINDANO YA MPIRA WA MIGUU KWA WAENDESHA BODA BODA, JIJINI DAR ES SALAAM

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na waendesha Pikipiki/Boda Boda (hawapo pichani) kabla ya kuzindua Mashindano ya Mpira wa Miguu kwa Waendesha Pikipiki katika Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, jijini Dar es Salaam. Mashindano hayo yajulikanayo kwa jina la Mpinga CUP yanatarajiwa kuanza kesho jijini humo. Katika hotuba yake, Masauni aliwataka waendesha Boda Boda jijini humo na nchini kwa ujumla kufuata sheria za usalama barabarani, na pia elimu ambayo wanapewa waitumie vizuri ili kuepuka ajali mbalimbali zinazosababishwa na uzembe wa madereva hao. Kushoto ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Naibu Kamishna, Mohamed Mpinga. Kulia ni Wafadhili wa Mashindano hayo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia) akimkabidhi mpira Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Naibu Kamishna, Mohamed Mpinga ikiwa ni ishara ya Naibu Waziri huyo kuzindua Mashindano ya Mpira wa Miguu kwa Waendesha Pikipiki katika Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, jijini Dar es Salaam. Mashindano hayo yajulikanayo kwa jina la Mpinga CUP yanatarajiwa kuanza kesho jijini humo. Katika hotuba yake, Masauni aliwataka waendesha Boda Boda jijini humo na nchini kwa ujumla kufuata sheria za usalama barabarani, na pia elimu ambayo wanapewa waitumie vizuri ili kuepuka ajali mbalimbali zinazosababishwa na uzembe wa madereva hao
Sehemu ya waendesha Boda Boda jijini Dar es Salaam, wakimsikiliza Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani) wakati kiongozi huyo alipokuwa anazungumza na madereva hao kabla ya kuzindua Mashindano ya Mpira wa Miguu kwa Waendesha Pikipiki katika Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, jijini humo. Mashindano hayo yajulikanayo kwa jina la Mpinga CUP yanatarajiwa kuanza kesho. Katika hotuba yake, Masauni aliwataka waendesha Boda Boda jijini Dar es Salaam na nchini kwa ujumla kufuata sheria za usalama barabarani, na pia elimu ambayo wanapewa waitumie vizuri ili kuepuka ajali mbalimbali zinazosababishwa na uzembe wa madereva hao
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akilionyesha Kombe ambalo Mshindi wa Kwanza atakabidhiwa mara baada ya kumalizika Mashindano ya Mpira wa Miguu kwa Waendesha Pikipiki katika Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, jijini Dar es Salaam. Masauni ameyazindua mashindano hayo jijini Dar es Salaam leo. Wapili kushoto ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Naibu Kamishna, Mohamed Mpinga
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akiijaribu pikipiki mpya ambayo atakabidhiwa Mshindi wa Kwanza mara baada ya kumalizika Mashindano ya Mpira wa Miguu kwa Waendesha Pikipiki katika Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, jijini Dar es Salaam. Masauni ameyazindua mashindano hayo jijini Dar es Salaam leo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (aliyevaa koti) akimsikiliza Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Naibu Kamishna, Mohamed Mpinga wakati alipokuwa anazungumza na Waendesha Boda Boda (hawapo pichani), kabla ya Naibu Waziri Masauni kuzindua Mashindano ya Mpira wa Miguu kwa Waendesha Pikipiki katika Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, jijini Dar es Salaam. Katika hotuba yake, Kamanda Mpinga alisema Mashindano hayo ambayo yameshirikisha Wilaya za Temeke, Kinondoni na sasa Ilala yanatarajiwa kumalizika Septemba 18, 2016.

No comments: