Advertisements

Friday, August 12, 2016

Olimpiki Rio: Kocha wa Kenya arejeshwa nyumbani kwa udanganyifu

Mwanariadha Ferguson Rotich

Kocha wa timu ya riadha ya Kenya inayoshiriki michuano ya Olimpiki mjini Rio de Janeiro amerudishwa nyumbani kwa kosa la udanganyifu.

Mkuu wa Timu ya Olimpiki ya kenya, Kip Keino amesema John Anzrah aliigiza kama miongoni wa wakimbiaji wa mita 800, na kutoa sampuli ya mkojo kwa niaba ya mkimbiaji Ferguson Rotich.

Udanganyifu uligundulika na wakaguzi wa dawa za kusisimua misuli baada ya kuangalia picha za kitambulisho alichokuwa amevaa, ndipo walipogundua kuwa sura ya Bw Anzrah haeindani na mchezaji aliyefanya uchunguzi.

Mkuu wa Timu ya Olimpiki ya Kenya, Kipchoge Keino amesema uongozi wa timu yake hautavumilia tabia hiyo ingawa mpaka sasa hakuna hatua yoyote iliyotolewa dhidi ya Rotich.

Anzrah ni afisa wa pili kutoka kenya kurejeshwa nyumbani, wa kwanza akirudishwa kwa kosa la kuomba rushwa ili kuweza kukwepa upimaji wa matumizi ya dawa za kusisimua misuli.

Kumekuwa na idadi kadhaa ya wanariadha wa Kenya ambao walishindwa kufuzu vipimo vya matumizi ya dawa za kuongeza nguvu huku ni wiki iliyopita tu shirika la kupambana na matumizi ya dawa hizo WADA likiiondoa Kenya kwenye nchi zilizoshindwa kutimiza masharti.

BBC

No comments: