Advertisements

Monday, August 1, 2016

TANZIA: KAMISHNA MSTAAFU WA MAGEREZA EGNO KAMILIUS KOMBA AFARIKI DUNIA JIJINI DAR

Marehemu Kamishna Mstaafu wa Magereza, Egno Kamilius Komba 

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini - CGP. John Casmir Minja anasikitika kutangaza kifo cha aliyekuwa Kamishna Mstaafu wa Sheria na Utawala wa Magereza - CP(Rtd) Egno Kamilius Komba kilichotokea jana Julai 31, 2016 akiwa nyumbani kwake Mvuti, Chanika Jijini Dar es Salaam.

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza anatoa pole kwa Watumishi wote wa Jeshi la Magereza nchini, familia ya Marehemu na wale wote walioguswa na msiba huu kwa namna tofauti tofauti.

Jeshi la Magereza kwa kushirikiana na familia ya Marehemu linaendelea kuratibu shughuli za msiba huo na taarifa za mazishi zitatolewa baadaye baada ya taratibu zote kukamilika.

Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi Amina.

No comments: