Advertisements

Sunday, August 28, 2016

WAZIRI JENISTA ATOA SOMO ​KWA ​MAB​E​​​​NKI, FINCA YAPETA


Sekta za kifedha zinazohusika na utoaji wa mikopo nchini zimetakiwa kutenga utoaji wa mikopo kwa wajasiriamali wa wadogo, kati na wakubwa ili kuleta unafuu wa masharti ya ukopaji. Hayo yalisemwa katika kilele cha mafunzo ya Wiki ya Huduma ya Kifedha na Uwekezaji na Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Jenista Mhagama alipokuwa anafunga siku ya mwisho ya mafunzo hayo Agosti 27.

Mhagama alisema kuwa mafunzo kwa wajasiriamali yamekuwa yakitolewa mara kwa mara ila kikwazo kimekuwa ni mkopo hususani kwa wajasiriamali wanaoenda kukopa masharti wanashindwa yakiwemo uwekaji wa hati ya nyumba kama dhamana na riba kubwa.

“Tanzania kuna takribani wajasiriamali milioni tano, ila wengi wao wanashindwa kupiga hatua kutokana na masharti mazito ya mikopo, mfano mama anauza vitumbua unamwamabia alete hati ya nyumba na wakati kapanga chumba kimoja” Alisema Mhagama.


Alieleza kuwa banki na wadau wote wa maendeleo wakutane ili kujadili ni namna gani wanavyoweza kupunguza masharti kwa wajasiriamali wadogo ili kuwakomboa na kupunguza tatizo la ajira na umasikini nchini. Mhagama ambae pia ni Mbunge wa Peramiho alisema kuwa Serikali itakuwa tayari kufanya majadiliano kuona namna ya kumsaidia mjasiriamali mdogo na wa kati huku akiwapongeza Banki ya Finca kwa kupunguza gharama za ukopaji kwa wananchi.

Meneja Masoko na Afisa Mahusiano wa Bank ya Finca, S pacio Aboubakar alisema walijitahidi kufatilia vikwazo vyote vinavyowakwamisha wajasiriamali na kuvifanyia kazi na kwa sasa kuna unafuu mkubwa wa masharti kwa mkopaji na ulipaji wa riba. Banki ya Finca imekuwa mkombozi kwa wajasiriamali nchini katika maonyesho hayo walifanikiwa kusajili zaidi ya wajasiriamali 4000 wapya.

Katika mafunzo hayo wajasiriamali kutoka vikundi mbalimbali vilishiriki ikiwemo Vikoba pia washindi walikabidhiwa fedha taslimu laki tano
​ ​
ili kuwapa motisha wajasiriamali wengine kushiriki miaka inayofata. Nuru Salim ni mmoja wa washindi wa zoezi lililofanywa na banki ya Finca na kuibuka mshindi alisema wamama wajitokeze kwa wingi kujifunza na kupata elimu ya uwekezaji na ujasiriamali ili kuepukana na tatizo la kuwa tegemezi.

“Mimi najihusisha na uuzaji wa nguo za wanawake Kariakoo, ila hapohapo nauza vitafunwa ninavyotengeza mwenyewe kama vitumbua ila nimekuja hapa kuongeza vitu vipya” Aleleza Nuru.

Maonyesho hayo yalikuwa ya tano na huwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta za banki, bima na uwekezaji kutoa elimu kwa wajasiriamali zaidi ya 20,000 na muitikio mkubwa ulikuwa wa wamama kuliko vijana na wanaum

No comments: