Advertisements

Wednesday, August 31, 2016

YALIOJIRI MKUTANO WA NCHI ZA JUMUIYA YA MADOLA KANDA YA AFRIKA NCHINI MAURITIUS

Viongozi Wakuu pamoja na Sekretieti ya Mkutano huo wakiwa katika picha ya pamoja baada ya ufunguzi wake, katikati  mwenye suti Waziri Mkuu wa Mauritius Sir Anerood Jugnauth. 
Ujumbe wa Tanzania walioshiki Mkutano huo wakiwa katika picha ya pamoja na Spika wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, Mhe Zuberi Ali Maulid katikati kulia Mwenyekiti wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Mussa Zungu  na kushoto Dk Raphael Chegeni. Kutoka kushoto Maryam Rajab, Mbarikiwa Masinga, Mhe, Maria (MB) Mhe. Raphael Chegeni (MB)Mhe Juma Hamad Omar (MB) Mhe Simai Mohammed Said (BLW)  Aziza Makwai.  
 
 Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe Zuberi Ali Maulid akibadilishana mawazo na Wajumbe kutoka Tanzania  kabla ya kuaza kwa Mkutano huo.


Mjumbe wa Mkutano wa Nchi za Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika Mhe. Simai Mohammed Said, akiwasilisha Mada wakati wa Mkutano huo inayozungumzia Suala la Nishati kwa Bara la Afrika, uliofanyika nchini Mauritius Balaclava. 
Spika wa Baraza la Wawkilishi Zanzibar Mhe. Zuberi Ali Maulid akiwa na Wajumbe kutoka Tanzania wakishirika katika Mkutano huo wakifuatilia Mada zinazowasilishwa na Wajumbe wakati wa Mkutano huo nchini Mauritius
Mtoto wa Mfalme wa Lesotho HRH Prince Seeiso B Seeiso, Raisi wa Senate na Mwenyekiti wa Kamati ya Biashara kutoka Bunge la Falme ya nchi ya Lesotho akichangia mada iliyowasilishwa na Tanzania inayohusiana na nishati ya umeme. 
 Mjumbe wa Sekterieti kutoka Tanzania Aziza Mwakwai kushoto akimsaidia Spika wa Rwanda wakati wa Kikao hicho za kuwasilisha Mada kwa Nchi husika. 
 Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe Zuberi Ali Maulid na Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said wakipitia makabrasha yao kabla ya kuaza Kikao cha Kanda ya Afrika Mashariki. katika ukumbi wa Hoteli ya Meridian Mauritius

Mjumbe wa Mkutano wa Nchi za Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika Mhe. Simai Mohammed Said akizungumza na Spika wa Bunge la Mauritius na Rais wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika Hon Mrs.Santi Bai Hanoomanjee. kulia kwake Katibu wa Bunge la Mauritius. 
Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe Zuberi Ali Maulid kutoka kulia akiwa katika picha ya pamoja na Spika wa Kenya Mhe.Justin Muturi, Spika wa Uganda Mhe Rebecca Kadaga na Mwenyekiti wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mussa Zungu akimwakilisha Spika wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Job Ndungai. 
 Spika la Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Zuberi Ali Maulid (katikati) akifurahia jambo wakati wakibadilishana mawazo na Wajumbe wa Mkutano huo, kushoto Spika wa Bunge la Uganda Mhe. Rebecca Kadaga na Mhe Simai Mohammed Said Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar, wakiwa nje ya Ukumbi wa Mkutano baada ya kuahirishwa kwa mapumziko ya mchana.
Katibu wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano la Tanzania ambaye pia Katibu wa Nchi za Jumuiya ya Madola Dk Thomas Kashillilah wa tatu kutoka kulia mwenye suti, akizungumza na Wajumbe wa Sekterieti ya Jumuiya ya Kanda ya Afrika wakiwa nje ya Ukumbi wa Mkutano huo uliofanyika Nchini Mauritius. 
Mwakilishi kutoka Zanzibar Mhe Simai  Mohammed Said akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Mkutano huo, pamoja na Spika wa Bunge la Kenya Mhe Justin Muturi mwenye kaunda suti pamoja wa Wawakilishi kutoka Kisiwa cha Rodrigues Mauritius.
Waziri wa Afya kutoka Nchini Botswana Hon Dorcas Makgato akiwa na Mjumbe kutoka Tanzania Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said wakiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu. 
Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe Zuberi Ali Maulid akiwa na Mhe Simai Mohammed Said wakiwa katika eneo maarufu la Kitalii nchini lijulikanali kwa jina la Trou Aux Cerfs (Valcano in Vacoas - Phoenix, Mauritius).
Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe.Zuberi Ali Maulid akiwa na Wajumbe wa Mkutano huo wakitembelea Kiwanda cha Kufulia Umeme na Sukari Nchini Mauritius wakipata maelezo kutoka kwa Kiongozi wa Kiwanda hicho cha Omnicane Limited. 
 Msanii wa Sanaa za kutengeneza Boti kwa ajili ya Watalii wanaotembelea Nchi hiyo akiwa katika harakati za kutengeza za boti zinazopatika katika eneo la Curepipe Mauritius hutengenezwa kwa mbao kama majahazi ya Zanzibar. 


 Sanamu la pili refu duniani baada la Nchini India lijukanali kwa jina Lord Shiva Nchini Mauritius likiwa katika maeneo ya Ganga Talao.
Mandhari ya kutoka juu ya bustani ya Trou Aux Cerfs.
Imetayarishwa na Zanzinews.com

No comments: