Advertisements

Saturday, September 3, 2016

BALOZI WILSON MASILINGI ATEMBELEA CHUO CHA MTANZANIA WINSTON SALEM, NC


Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi akitia saini kitabu cha wageni katika chuo kinachomilikiwa na Mtanzania Dr. Lucas Shallua kilichopo Winston Salem, North Carolina siku ya Ijumaa Septemba 2, 2016.

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi akifanya mazungumzo na mmiliki wa chuo cha Mount Eagle College &University Dr. Lucas Shallua siku ya Ijumaa Septemba 3, 2016 Balozi Wilson Masilingi alipotembelea chuo hicho kilichopo Winston Salem, North Carolina.
 Mazungumuzo yakiendelea, wengine katika kufuatilia mazungumuzo hayo kutoka kushoto ni ni Afisa Uhamiaji wa Ubalozi Bwn. Abbas Missana, Dr. Dorothy Edward Shallua (mke wa Dr. Lucas Shallua), Mke wa Balozi Marystela Masilingi, na mwenyeiki wa Umoja wa Watanzania North Carolina, Bi. Gloria Alex.
 Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi akimsikiliza Dr. Lucas Shallua alipokua akimwonyesha moja ya darasa linalotumia kurekodia masomo ya matandaoni.
 Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi akimsikiliza Dr. Lucas Shallua (kulia) alipokua amkitembeza na kumwonyesha chuo cha Mount Eagle College & University kilichopo mji wa Winston Salem, North Carolina. Wengine katika picha kutoka kushoto ni mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Watanzania North Carolina, Bi. Gloria Alex, Mke wa Balozi Bi. Marystela Masilingi, nyuma ya Balozi asiyeonekana ni Afisa Uhamiaji wa Ubalozi Bwn. Abbas Missana na Mke wa Shallua, Dr. Dorothy Edward Shallua.
 Moja ya madarasa chuoni hapo.
 kutoka kushoto ni Afisa Uhamiaji wa Ubalozi Bwn. Abbas Missana, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Watanzania North Carolina, Bi. Gloria Alex, nyuma ya Mhe. Balozi ni mkewe Marystela Masilingi, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi, mke wa Shallua, Dr. Dorothy Edward Shallua na Dr. Lucas Shallua ambaye akitoa maelezo kwa Mhe. Balozi wakati akimtembeza na kumwonyesha chuo hicho.
 Mke wa Dr. Shallua, Dr. Dorothy Edward Shallua (kulia) akimuelezea Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi kuhusiana na kampuni yake ya Mount Eagle Health Care ambayo ofisi zake pia zipo kwenye jengo la ofisi za chuo hicho.
 Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi akisikiliza maelezo kutoka mmoja ya walimu wa darasa la utgawaji utumiaji wa dawa kwa mgonjwa chuoni hapo Mwl. Allen Greene (kushoto) kati ni Dr. Lucas Shallua akifuatilia kwa makini muzungumuzo hayo.
 Wapili toka kushoto ni Mkuu wa chuo Bi. Denese Methews akitoa maelezo kwa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi (watano toka kushoto) kuhusiana na chuo hicho wengine wanao msikiliza kutoka kushoto ni mke wa Dr. Shallua, Dr. Dorothy Edward Shallua, mwenyeki wa Jumuiya ya Umoja wa Watanzania North Carolina, mke wa Balozi, Marystela Masilingi na Dr. Lucas Shallua.
 Kutoka kushoto ni Ted, mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Watanzania North Carolina Bi. Gloria Alex, Mke wa Balozi Marystela Masilingi, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi, Dr. Lucas Shallua, mke wa Dr. Shallua, Dr. Dorothy Edward Shallua na Afisa Uhamijai wa Ubalozi, Bwn. Abbas Missana.
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi na mkewe wakipokea zawadi kutoka mke wa Dr. Shallua, Dr. Dorothy Edward Shallua na Dr. Lucas Shallua.

Chuo cha Mount Eagle kinatoa unafuu kwa Mtanzania anayetaka kujiunga katika masomo ya Unesi na ugawaji dawa na chuo hicho kwa kukuwezesha wewe kufanyakazi hospitanini au kwenye maduka ya dawa pia wanamsomo ya mtandaoni kwa bei nafuu. Kwa maelezo zaidi usisite kuwasiliana na Dr. Lucas Shallua barua pepe Lshallua@mounteag.com 

No comments: