Advertisements

Friday, September 2, 2016

MGODI WA DHAHABU WA BULYANHULU UMETANGAZA KUTOA MILIONI 100 KWA AJILI YA MADAWATI MKOA WA GEITA

Naibu Waziri wa TAMISEMI Sulemani Jafo akihutubia wadau wa kampeni ya kuchangia Madawati Mkoa wa Geita kwenye Harambee iliyofanyika Mjini Geita
Meneja wa Ustawi na Mahusiano ya Jamii katika Mgodi wa Acacia Bulyanhulu Elias Kasitila akitoa maelezo kuhusu namna Acacia ilivyoshiriki mwaka huu kuchangia kwenye zoezi la madawati.
      Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Acacia Bulyanhulu Bwana Graham Crew akiwa amenyoosha mikono kusalimia umma wa Watanzania waliongana kwenye harambee ya madawati Geita
Timu ya Wafanyakazi wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri baada ya Meneja wa Ustawi na Mahusiano ya Jamii katika Mgodi wa Acacia Bulyanhulu Elias Kasitila kutanga kuwa Mgodi utatoa shilingi milioni Mia Moja kwa ajili ya madawati Mkoa wa Geita.

Na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog.

Mgodi wa Dhahabu Bulyanhulu  Umetoa Tsh 100m/- kwa Ajili ya Madawati ya Shule Mkoani Geita. 


 Akitangaza kiwango hicho katika hafla ya changizo iliyofanyika  Desire Park Mjini Geita , Meneja Ufanisi na Mahusiano na Jamii wa Mgodi wa Dhahabu  Bulyanhulu bwana Elias Kasitila amesema, “Bulyanhulu  imebarikiwa kuwa  karibu na Wilaya mbili,Halmashauri ya Msalala iliyopo Mkoa wa Shinyanga na Nyang’wale iliyopo Mkoa wa Geita.

“ Hivyo basi tulipopokea  mwaliko kutoka  kwa Mkuu wa wilaya ya  Nyang’wale  kuhusu kampeni ya leo  ya madawati tumeamua kwamba japokuwa  miradi mingine ya madawati tumeifanya mkoa wa Shinyanga tumeona kuna umuhimu  wa kufanya hivyo  mkoa wa Geita pia.”alisema Kasitila.

"Hivyo basi  siku ya leo tunajitolea  kuchangia Tsh100m/- kwa ajili ya kampeni  za mikoa inayolenga kuondoa  upungufu wa  madawati 70,000.”aliongeza Kasitila.


 Elias aliongeza kuwa, “misaada ya madawati kutoka kwenye migodi iliyoko chini  ya Acacia ambayo ni, North Mara, Buzwagi and Bulyanhulu,kwa mwaka huu Acacia imetumia  takriban fedha za kitanzania zaidi ya Billion Moja  ambayo inakadiliwa kutengeneza zaidi ya madawati 10,000.

 Mgeni rasmi katika hafla ya kuchangia madawati mkoa wa Geita alikuwa Waziri Mkuu wa  Tanzania Mh. Kassim Majaliwa ambaye aliwakilishwa na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi ,Utumishi na Utawala Bora, Mh.Suleiman Jafo.

 Akiwahutubia  washika dau waliokuwa  Desire park Naibu Waziri Jafo  alisema “Nitapeleka salamu kwa waziri mkuu  kuhusiana na mwitikio ambao nimeushuhudia leo  ninaagiza kamati ya Kampeni ya madawati Geita kuorodhesha washika dau wote waliochangia  leo na kuwasilisha orodha hiyo kwenye ofisi ya Waziri Mkuu ili binafsi awatambue wote walioonesha kuguswa kuiondolea Geita uhaba wa madawati.”

 Katika hafla hiyo Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Aacacia Bulyanhulu Graham Crew binafsi alijitolea kuchangia  fedha za kitanzania shilingi 750,000/- kwa ajili ya kampeni hiyo.

No comments: