Advertisements

Friday, September 9, 2016

RAJAB NA KITHARA TAARAB WATUMBUIZA WASHINGTON, DC

Kundi zima la Rajab and Kithara Taarab lenye kupiga mziki wa mahadhi ya mwambao kutoka Zanzibar, walipotumbuiza siku ya Jumanne Sept 6. ndani ya ukumbi wa The John F. Kennedy Center for the Performing Arts Jijini Washington.  Rajab and Kithara watakua hapa Marekani mwezi mzima wakitumbuiza States mbali mbali hapa Marekani. kwa ratiba zao bofya hapa  centerstageus.org

Mmoja wa waimbaji wa kundi zima la Rajab and Kithara,  Saada Nassor, akitumbuiza wimbo wa Chungu,  ndani ya ukumbi wa The John F. Kennedy Center for the Performing Arts  iliopo Jijini Washington. (Picha zote na swahilivilla.blogspot.com)
Saada Nassor, akionyesha pozi wakati anawatumbuzia Wamarekani.

Makame Faki  akitumbuiza wimbo wa "Salaam Aleikum"
 
Makame Faki  akiimbaa wimbo wa "Salaam Aleikum"
Wataalamu wa upigaji wa vyombo vya mahadhi ya mwambao,  mpiga ngoma Foum Faki, (kushoto) akiwa na  mpiga bass kitaa,  Daudi Shahil, wakitumbuiza  wageni waalikwa 
Kundi zima la Rajab and Kithara Taarab,  Zanzibar walivyotumbuiza Jijini Washington 
 Mtaatam wa wa quanun Zanzibar ambae pia ni kiongozi wa kundi zima la  Rajab and Kithara, Rajab Suleiman akitambulisha kundi zima la Rajab and Kithara.  Picha  zaidi Bofya hapa

No comments: