Advertisements

Tuesday, September 13, 2016

TASWIRA MBALIMBALI KUTOKA BUNGENI MJINI DODOMA LEO

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson akiongoza sala wakati wa ufunguzi wa kikao cha Bunge leo Mjini Dodoma.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo akijibu wakati wa kikao cha bunge ambapo alisema serikali ipo katika uhakiki wa maombi ya maeneo mapya utawala kwa kuangalia vigezo katika kuanzisha maeneo hayo.
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akijibu wakati wa kikao cha bunge ambapo alisema serikali serikali itaendelea kuongeza udahili wa walimu wa sayansi katika vyuo vya elimu ili kuweza kukidhi mahitaji husika.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo (kushoto) akimueleza jambo Waziri Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Mhe. George Simbachawene.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akijibu wakati wa kikao cha bunge ambapo aliwaeleza wabunge kuwa Katiba ya Nchi ibara ya 3(2) inaeleza kuwa mambo yote yanayohusu uandikishaji na uendeshaji wa vyama vya siasa nchini yatasimamiswa kwa mujibu wa masharti ya katiba na sheria iliyotungwa ba Bunge
Waziri Wizara ya Mmabo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mwigulu Nchemba akijibu wakati wa kikao cha bunge ambapo alisisitiza watanzania kufuata sheria za nchi na iwapo utakiuka jeshi la polisi litachukuwa hatua bila kujali itikadi ya chama chochote cha siasa.
Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijini Mhe. John Heche akichangia hoja kuhusu tetemeko la ardhi mkoani Kagera wakati wa kikao cha Bunge leo Mjini Dodoma.
Mbunge wa Jimbo la Muleba Kusini Mhe. Prof. Anna Tibaijuka akichangia hoja kuhusu tetemeko la ardhi mkoani Kagera wakati wa kikao cha Bunge leo Mjini Dodoma ambapo mbali na mambo mengine wabunge wamekubaliana kuchangia posho ya siku moja kwa ajili ya wahanga wa tetemeko mkoani Kagera.
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakisimama kwa dakika moja kuungana na wahanga wa tetemeko lililotokea mkoani Kagera.
Waziri Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Mhe. George Simbachawene akitoa taarifa ya serikali kuhusu tetemeko la ardhi lililotokea hivi karibuni Mkoani Kagera. PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO

No comments: