Advertisements

Tuesday, September 13, 2016

TETEMEKO LA ARDHI MKOANI KAGERA LAPELEKEA SHULE ZA SEKONDARI ZA IHUNGO NA NYAKATO KAFUNGWA KWA MUDA

Shule ya Sekondari Ihungo iliyoko mjini Bukoba huko Kagera yafungwa hadi Septemba 26 baada ya miundombinu kuharibiwa na tetemeko la ardhi, diwani wa kata ya Nshambya Jimmy Karugendo athibitisha leo asubuhi.
Mwenyekiti wa taifa wa chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe aliishauri serikali kuifunga shule ya sekondari ya Ihungo ambayo imepata madhara makubwa kutokana na tetemeko la ardhi lilitokea mkoani Kagera na kuunda kamati ya kitaifa ya maafa itakayoshughulikia madhara yaliyotokana tetemeko hilo liliyoyakumba maeneo mbalimbali yaliyoko katika mkoa huo.
Alitoa kauli hiyo baada ya kujionea madhara yaliyotokana na tetemeko hilo katika shule hiyo hali inayowalazimu wanafunzi kulala kwenye uwanja na madhara ya nyumba za makazi ambazo zimeharibika vibaya na nyingine kuanguka kabisa, amesema madhara ya tetemeko hilo serikali inapaswa kuyachukulia kama moja ya majanga la kitaifa.

No comments: