Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) umetangaza kusogeza mbele kwa siku moja safari ya treni ya abiria ya Jumanne kwenda bara kutoka Dar es Salaam. Treni hiyo itaondoka Jumatano Septemba 14, 2016 saa 9 alasiri.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo sababu za kusogezwa mbele ni kutokana na kipande cha treni kuitoka Kigoma kuchelewa kufika Tabora. Treni hiyo wakati ikienda Kigoma ilicheleweshwa kufika Kigoma baada ya treni ya mizigo kupata ajali kati ya stesheni za Kazuramimba na Luiche..
Uongozi wa TRL unawaomba radhi abiria na wananchi kwa ujumla kwa usumbufu utakaojitokeza
Atakayesoma taarifa hii amwarifu mwenzake.
Imetolewa na Afisi ya Uhusiano kwa niaba ya
Mkurugenzi Mtendaji wa TRL,
Ndugu Masanja Kungu Kadogosa
Dar es Salaam,
Septemba 12, 2016
No comments:
Post a Comment