Advertisements

Saturday, September 3, 2016

Usajili wa MeTL Career Fair (Job Bonanza) kufungwa leo jumamosi changamkia fursa

Kama wewe ni mhitimu katika Uhandisi au Utawala (Masoko, Mahusiano, Fedha) na una hari ya kujifunza, ukiwa na mtazamo chanya wa mafanikio na mfuatiliaji wa maadili katika kazi, njoo ujiunge nasi katika bonanza hili la uchambuzi wa ajira.
Rasilimali Watu
Mauzo
Uhasibu
Masoko
Uhandisi
Kilimo
Nguo

Kwani unaweza ukawa mmoja kati ya watu 25 tutakaowachagua kwa ajili ya kujiunga kwenye programu ya uendelezaji wa wahitimu wa vyuo vikuu.
Na ukibahatika kuwa mmoja wapo kati ya hao utapata nafasi ya kujifunza kwa vitendo katika viwanda vyetu vilivyopo maeneo mbalimbali.
Pia utapata nafasi ya kufundishwa mifumo ya uendeshaji wa viwanda vya kisasa.
Utakuwa chini ya wakufunzi waliobobea katika kazi zao duniani ambao watakuwezesha wewe kukua katika kazi na kushika nyadhifa kwenye kazi yako.
Zaidi ya yote hayo utakayofanyiwa pia utalipwa ilikujifunza

Kwa taarifa zaidi tazama vipeperushi vyetu:

No comments: