Advertisements

Thursday, October 13, 2016

KONGAMANO LA HAKI YA AFYA YA UZAZI LAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM

Mkurugenzi wa Huduma za Sheria kwa Umma Bw. Justus Mulokozi akifungua kongamano la Kitaifa la Haki ya Afya ya Uzazi katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya New Africa jijini Dar es salaam ambapo wadau mbalimbali wamehudhuria katika kongamano hilo wakiwemo Wanasheria , Wanasiasa, Wanafunzi Waandishi wa habari pamoja na waalikwa mbalimbali.
Mkurugenzi wa Chama cha Wanasheria Wanawake TAWLA Bi. Tike Mwambipile akizungumza katika kongamano hilo wakati alipokuwa akifafanua mambo mbalimbali kuhusu Haki ya Afya ya Uzazi.
Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mama Anne Makinda akiwa katika kongamano hilo pamoja na washiriki wengine kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Huduma za Sheria kwa Umma Bw. Justus Mulokozi, Mwenyekiti wa TAWLA Bi. Attanasia Soka na Jaji Winnie Korosso.
Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria Wanawake (TAWLA) Bi. Attanasia Soka na Jaji Winnie Korosso akimkaribisha mgeni rasmi ili kufungua kongamano hilo.
Baadhi ya wanasheria wanawake na wageni waalikwa kutoka taasisi mbalimbali wakiwa katika kongamano hilo.
Kutoka kulia Mgeni rasmi katika Kongamano hilo Mkurugenzi wa Huduma za Sheria kwa Umma Bw. Justus Mulokozi, akiwa na Mkurugenzi wa TAWLA Bi. Tike Mwambipile na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Bi. Pindi Chana.
Watoa mada wa kongamano hilo wakifuatilia kongamano hilo.
Baadhi ya wadau mbalimbali katika picha tofauti wakionekana kufuatilia na kuandika mambo muhimu yanayojadiliwa katika kongamano hilo.
Mkurugenzi wa Chama cha Wanasheria Wanawake TAWLA Bi Tike Mwambipile akiwa katika picha ya pamoja na Nasieki Kisambu Kutoka TAWLA na Salome Argan Mtoa mada wa Kongamano hilo kutoka Legal Advicer For Africa Center for Reproductive Rights.
Mkurugenzi wa Chama cha Wanasheria Wanawake TAWLA Bi Tike Mwambipile akifurahia jambo na Jaji Winnie Korosso.

No comments: