Advertisements

Tuesday, November 1, 2016

Viongozi wa Democratic wamkosoa mkuu wa shirika la upelelezi

Bi Clinton amesema kuwa alikuwa na uhakika kwamba shirika hilo la upelelezi lingesema hivyohivyo kwa mara nyingine

Ikulu ya Marekani imeingia katika mgogoro ambao umetikisa kampeni za urais, katika hatua za kufunga kampeni hizo.

Rais Obama amesema hamuamini mkurugenzi wa shirika la upelelezi nchini humo, James Comey,na kuwa anajaribu kushawishi matokeo ya uchaguzi huo.

Viongozi wa juu wa Democratic wamemkosoa vikali Bwana Comey baada ya shirika la upelelezi wiki iliyopita kusema kuwa lilikuwa likichunguza iwepo wa barua pepe mpya zilizogunduliwa zaweza kumuhusu Bi Clinton.

Shirika hilo limeongeza kuwa wanachunguza ili kuona iwapo zimejumuisha taarifa za siri.

Mapema uchunguzi wa shirika la upelelezi la Marekani lilisema kuwa watumishi wa barua pepe binafsi ya Bi Clinton walizifuta barua za makosa ya kihalifu za Bi Clinton.

Akiongea mjini Ohio, Bi Clinton amesema kuwa alikuwa na uhakika kwamba shirika hilo la upelelezi lingesema hivyohivyo kwa mara nyingine.

BBC

No comments: