Advertisements

Saturday, December 3, 2016

MWALIMU AFARIKI KATIKA MKUTANO WA CHAMA CHAO CHA CWT JIJINI DAR ES SALAAM

 Mwalimu Tuhobwike Mwinuka Mwakatumbula enzi za uhai wake.
 Jeneza lenye mwili wa mwalimu Tuhobwike Mwinuka Mwakatumbula likiwa ndani ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Wazo Hili Dar es Salaam leo asubuhi wakati wa ibada ya kuuaga mwili huo.
Binamu wa marehemu, Nobert Nselu (kulia) akimsaidia rafiki wa karibu wa marehemu mama Malugu wakati mwili wa marehemu ukiwasili nyumbani kwake.
 Rafiki wa marehemu mama Malugu (katikati) akisaidiwa.
 Waombolezaji wakiwa msibani nyumbani kwa marehemu 
Wazo Hill.


 Ni huzuni kubwa 
 Wakina mama wakiwa na maua wakati wakisubiri mwili wa marehemu kuingizwa ndani.
 Geneza lenye mwili wa marehemu likiingizwa nyumbani kwake. 
 Mtoto mkubwa wa marehemu Nico Mwakatumbula (katikati), akisaidiwa baada ya kutoa heshima za mwisho kwa mama yake.
 Waombolezaji wakiingiza jeneza lenye mwili wa marehemu katika Kanisa la KKKT Usharika wa Wazo Hill.
 Mwili ukiwa kanisani.
 Mume wa marehemu akiwa na watoto wake. Kutoka kulia ni Gloria, Kelvin na Nico.
 Wanafamilia wakiwa katika ibada hiyo ya kumuaga mpendwa wao.
 Waumini wa kanisa hilo wakiwa kwenye ibada hiyo.N a Dotto Mwaibale

MWALIMU Tuhobwike Mwinuka Mwakatumbula wa Shule ya Msingi Kumbukumbu katika Manispaa ya Kinondoni amefariki dunia wakati akiwa katika mkutano wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) na viongozi wa Idara ya Elimu wa manispaa hiyo.

Kifo cha mwalimu huyo kimetokea Desemba 1, 2016 Siku ya Ijumaa majira ya jioni wakati viongozi hao walipokuwa wakimalizia ziara yao ya kutembelea shule mbalimbali katika manispaa hiyo.

Akizungumza na Jambo Leo mume wa marehemu Samuel Mwakatumbula alisema mke wake hakuwa na tatitizo lolote la kiafya na siku ya tukio hilo aliamka salama na kumuaga kuwa anawahi kwenye mkutano huo.

"Siku chache kabla ya kifo chake mke wangu aliniambia alikuwa hajisikii vizuri kwani alikuwa na uchovu wa kawaida" alisema Mwakatumbula.

Mwakatumbula alisema alipigiwa siku na kuambiwa kuwa mke wake alianguka ghafla wakati mkutano ukiendelea na kupoteza fahamu ambapo alikimbizwa Hospitali ya Mount Mkombozi iliyopo maeneo ya Morocco ambapo waliambiwa tayari alikuwa amefariki.

Mwili wa marehemu ulisafirishwa jana kwenda Kiwira wilayani Rungwe mkoani Mbeya kwa maziko yatakayofanyika leo marehemu ameacha mume na watoto watatu, Nico, Kelvin na Gloria.

No comments: