Advertisements

Wednesday, December 7, 2016

RAIS SHEIN AONGOZA MAHAFALI YA CHUO KIKUU CHA TUNGUU ZANZIBAR


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi wakati alipowasili katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Tunguu (Zanzibar University) Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja akiwa mgeni rasmi katika Mahafali ya Kumi na nne yaliyofanyika Chuoni hapo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akitoa hutuba yake wakati wa sherehe ya mahafali ya kumi na nne (14) katika Chuo Kikuu cha Tunguu (Zanzibar University) Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja, (kulia) Prof.Saleh Idriss Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo na (kushoto) Mkuu wa Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu, pia Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Prof.Suleiman Bin- Nassry Basahal.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipokea zawadi kutoka wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu, pia Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Prof.Suleiman Bin- Nassry Basahal wakati wa sherehe ya Mahfali ya kumi na nne iliyofanyika leo katika Chuo hicho huko Tunguu Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.
Baadhi ya wahitimu katika Mahafali ya kumi na nne (14) ya Chuo Kikuu cha Tunguu (Zanzibar University) wakiwa katika sherehe za Kutunukiwa Vyeti,Diploma,Stashahada,na Shahada na nyenginezo zilizofanyika leo katika viwanja vya Chuo hicho Tunguu Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja,mgeni rasmi akiwa Rais Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(hayupo pichani).
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu,pia Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Prof.Suleiman Bin- Nassry Basahal alipokuwa alipokuwa akiwatunuku Stashahad na Shada wahitimu katika fani mbali mbali wa mwaka 2016 wakati wa sherehe ya Mahafali ya kumi na nne yaliyofanyika leo katika Chuo hicho huko Tunguu Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.
Baadhi ya waalikwa mbalimbali waliohudhuria katika sherehe za mahafali ya kumi na nne katika Chuo Kikuu cha Tunguu (Zanzibar University) Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja yaliyofanyika leo, mgeni rasmi akiwa Rais Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dk.Ali Moahmed Shein.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akifuatana na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu, pia Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Prof. Suleiman Bin- Nassry Basahal (kulia) baada ya kumalizika kwa sherehe ya Mahafali ya kumi na nne yaliyofanyika leo katika Chuo hicho huko Tunguu (Zanzibar University) Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja,wengine (kushoto)Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Dkt. Adissa Muslim Hija na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiwapungia mkono wananchi mbalimbali na Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu ,wakati wa sherehe ya Mahafali ya kumi na nne yaliyofanyika leo katika Chuo hicho huko Tunguu (Zanzibar University) Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja leo. (Picha na Ikulu)


No comments: