Advertisements

Monday, January 16, 2017

MAGARI YA SERIKALI YENYE MAKOSA KUTOZWA FAINI

Kamanda wa Polisi Kikosi cha usalama Barabarani, Mohamed Mpinga amesema kumekuwepo na malalamiko mengi kuwa magari ya serikali yanapendelewa hivyo kutawekwa kamera katika barabara kuu ili kupiga picha magari yote yenye makosa na kuadhibiwa.

Kamanda Mpinga ameyasema hayo katika mahojiano maalumu na Gazeti la Mwananchi na kusema kwa kipindi cha January hadi Disemba mwaka jana makosa yaliyotokea nchini ni milioni 1.9.
“Kamera hizo hazitajali ni gari la waziri, serikali, wala Mpinga na zitapiga picha gari zote kama ilivyo kwa msemo wa kupanga na kuchagua,”amesema Mpinga.
Aidha Mpinga alisema kuwa makosa hayo yalitokana na ulevi, mwendo wa kasi,kupita katika taa nyekundu,kukatisha safari na kutovaa kofia ngumu.

No comments: