Advertisements

Tuesday, January 17, 2017

MEJA JENERALI MSTAAFU MUHUGA AFUNGUA MAFUNZO KWA WACHIMBAJI MADINI WADOGO WATAKAONUFAIKA NA AMBAO HAWATANUAFAIKA NA RUZUKU YA AWAMU YA TATU.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Prof. James Mdoe (wa kwanza kushoto, waliosimama) akizungumza wakati wa mafunzo ya Wachimbaji Madini Wadogo Watakaonufaika na ambao hawatanufaika na Ruzuku ya Wachimbaji Madini Wadogo ya Awamu ya Tatu yaliyofanyika mjini Mpanda mkoani Katavi. Waliokaa mbele Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Meja Jenerali Mstaafu, Rafael Muhuga (wa pili kulia, Kaimu Kamishna wa Madini, Julius  Sarota, (wa tatu kulia), na Mtendaji Mkuu  wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Madini Wadogo Tanzania (FEMATA), Haroun Kinega, (wa kwanza kulia).
Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Meja Jenerali Mstaafu, Rafael Muhuga akifungua rasmi mafunzo ya Wachimbaji Madini Wadogo Watakaonufaika na ambao hawatanufaika na Ruzuku ya Wachimbaji Madini Wadogo ya Awamu ya Tatu yaliyofanyika mjini Mpanda mkoani Katavi.

Baadhi ya Wachimbaji Madini Wadogo watakaonufaika na Ruzuku ya Awamu ya Tatu inayotolewa na Serikali wakifuatilia mafunzo yaliyokuwa yakitolewa na Wataalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini mjini Mpanda mkoani Katavi.
Mhandisi Chacha Megewa kutoka Wizara ya Nishati na Madini  akitoa mafunzo kuhusu ujasiriamali na menejimenti ya uchimbaji mdogo wa madini kwa Wachimbaji Madini Wadogo watakaonufaika na Ruzuku ya Awamu ya Tatu na ambao hawatanufaika Ruzuku hiyo. Mafunzo hayo yalifanyika mjini Mpanda mkoani Katavi.
Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Meja Jenerali Mstaafu, Rafael Muhuga (wa tatu kulia waliokaa), Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Prof. James Mdoe (wa pili kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Wadau mbalimbali walioshiriki mafunzo ya Wachimbaji Madini Wadogo Watakaonufaika na ambao hawatanufaika na Ruzuku ya Wachimbaji Madini Wadogo ya Awamu ya Tatu yaliyofanyika mjini Mpanda mkoani Katavi. Wengine waliokaa mbele ni Kaimu Kamishna wa Madini, Julius  Sarota, (wa kwanza kulia), Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji Madini Wanawake nchini (TAWOMA), Eunice Negele (wa pili kulia) na Makamu wa Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Madini Wadogo Tanzania (FEMATA), Dkt. Omar Mzeru (wa kwanza kushoto).
Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Meja Jenerali Mstaafu, Rafael Muhuga (wa tatu kulia waliokaa), Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Prof. James Mdoe (wa pili kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Watendaji wa Taasisi mbalimbali na Makamishna Wasaidizi wa Madini wa Kanda mbalimbali walioshiriki mafunzo ya Wachimbaji Madini Wadogo Watakaonufaika na ambao hawatanufaika na Ruzuku ya Wachimbaji Madini Wadogo ya Awamu ya Tatu yaliyofanyika mjini Mpanda mkoani Katavi. Wengine waliokaa mbele ni Kaimu Kamishna wa Madini, Julius  Sarota, (wa kwanza kulia), Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji Madini Wanawake nchini (TAWOMA), Eunice Negele (wa pili kulia) na Makamu wa Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Madini Wadogo Tanzania (FEMATA), Dkt. Omar Mzeru (wa kwanza kushoto).
Kamishna Msaidizi wa Madini, Kanda ya Kusini, Mhandisi, Benjamin Mchwampaka (wa tatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wachimbaji Madini Wadogo watakaonufaika na Ruzuku ya Awamu ya Tatu kutoka Kanda hiyo ya Kusini.
Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Meja Jenerali Mstaafu Rafael Muhuga (wa tatu kulia waliokaa), Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Prof. James Mdoe (wa pili kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja watumishi wa Wizara ya Nishati na Madini walioshiriki mafunzo ya Wachimbaji Madini Wadogo Watakaonufaika na ambao hawatanufaika na Ruzuku ya Wachimbaji Madini Wadogo ya Awamu ya Tatu yaliyofanyika mjini Mpanda mkoani Katavi. Wengine waliokaa mbele ni Kaimu Kamishna wa Madini, Julius  Sarota, (wa kwanza kulia), Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji Madini Wanawake nchini (TAWOMA), Eunice Negele (wa pili kulia) na Makamu wa Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Madini Wadogo Tanzania (FEMATA), Dkt. Omar Mzeru (wa kwanza kushoto).

No comments: