Advertisements

Thursday, February 16, 2017

YUSUFU MANJI AFIKISHWA MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI KISUTU MCHANA HUU.

Mfanyabiashara maarufu nchini na mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Yusufu Manji amefikishwa mahakamani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Hivi sasa ameingizwa katika mahabusu ya mahakama, akisubiri kupandishwa kizimbani kusomewa mashtaka yanayomkabili.

Manji amefikishwa mahakamani leo ikiwa ni siku ya nane tangu alipojisalimisha na kushikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam, alopoitikia wito wa Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda ili kuhojiwa.

Umati mkubwa wa watu wanaodhaniwa kuwa ni mashahabiki wa Klabu ya Yanga, ndugu jamaa na marafiki wamefurika katika chumba cha mahakama, wakimsubiri apandishwe kizimbani.

No comments: