Advertisements

Monday, March 20, 2017

WAZIRI MWIGULU NCHEMBA AFANYA MAZUNGUMZO NA MWAKILISHI MKAZI WA WFP, JIJINI DAR ES SALAAM LEO

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba (kulia) akimkaribisha ofisini kwake Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) nchini, Michael Dunford kwa ajili ya kufanya mazungumzo naye kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya WFP na Tanzania. Mazungumzo hayo yalifanyika katika ofisi ya Waziri huyo, jijini Dar es Salaam leo.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba (kushoto) akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) nchini, Michael Dunford, wakati kiongozi huyo alipomtembelea Waziri Mwigulu, jijini Dar es Salaam leo, kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Shirika lake na Tanzania. Katikati ni Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi nchini, Harrison Mseke.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba (kushoto) akimsikiliza Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) nchini, Michael Dunford, wakati kiongozi huyo alipomtembelea Waziri Mwigulu, jijini Dar es Salaam leo, kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya WFP na Tanzania. Katikati ni Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi nchini, Harrison Mseke. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments: