Advertisements

Sunday, April 23, 2017

WATU WATATU WANAOTUHUMIWA KUHUSIKA NA MAUAJI YA VIONGOZI WA VIJIJI NA ASKARI MKOANI PWANI WAMEUAWA.

Jeshi la polisi mkoani Pwani limewaua kwa kuwapiga risasi watu watatu wanaodhaniwa kuwa wali husika na mauaji ya viongozi wa vijiji na vitongoji na askari polisi katika wilaya za Mkuranga,Kibiti na Rufiji.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani ONESMO LYANGA amesema katika taarifa yake kuwa watu hao wamefariki dunia wakati wakipelekwa hospitali ya Mission ya Mchukwi kwa matibabu baada ya kujeruhiwa kwa risasi miguuni na kiunoni walipojaribu kukimbilia porini wakiwa kwnye pikipiki baada ya kukaidi amri halali ya polisi iliyowata ka  wasimame kutokana na kuwatilia mashaka.

Amesema polisi waliokuwa katika doria walipata taarifa kutoka kwa wa safiri  kuwa waliona pikipiki tatu zilizokuwa zinatokea Kibiti kupitia barabara kuu ya Dar es salaam -Lindi zinepakia watu watatu kila mmoja na pikipiki mbili kati ya hizo ziliwabeba waliovalia hijabu ndipo walipowapa taarifa askari wa usalam barabararni walioko katika kizuizi cha Mparange ili wawasimamishe na kuwatambua lakini hawakutii.


Amesema askari wa kituo cha Mwembe,Muhoro waliwasinamisha lakini hawakutii amri na kuongeza kasi,ndipo askari waliwafuatilia hadi kuvuka daraja la Mkapa  na wakatoa onyo kwa kufyatua risasi hewani lakini waliendelea kukaidi.

Amesema baadaye watu hao waliamua kuruka kutoka kwenye pikipiki  zao na kukimbilia msituni,kitendo kilichowafanya polisi kuwafyatulua risasi za miguuni na kiunoni na kuwakamata lakini walifariki dunia wakati wakikimbizwa hospitali ya Mission ya Mchukwi ambako daktari alithibitisha watu hao walikuwa wameshafariki.

Kamanda amesema majeruhi hao waliovalia hijabu baadaye walitambukiw kuwa walikuwa wanaune waliotumia pikipiki aina ya BOXER yenye namba za usajili MC 272 BLW.

CHANZO: ITV TANZANIA

No comments: